Skip to main content

Tatizo La Kupoteza Kumbukumbu Alzheimer Disease

Kupoteza kumbukumbu ni ugonjwa unaoingia kwa kasi ugonjwa Umetajwa sasa unakuja juu kuliko maradhi sugu kama vile kisukari, shinikizo la damu, kiharusi na saratani
Kupoteza kumbukumbu hutokea pale eneo la ubongo linalohusika katika kuhifadhi taarifa linapoathirika.

Ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu kwa kawaida unawapata wazee. Uligunduliwa kwa mara ya kwanza mwaka 1906 na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Akili, Alois Alzheimer.

Dk Alzheimer, ambaye ni MjerumU ani, alipata mgonjwa mwenye tatizo hilo ambaye alikuwa anapoteza kumbukumbu, kuchanganyikiwa na kupata ugumu wa kuelewa maswali anayoulizwa.

Mgonjwa huyo alifariki dunia na ndipo Dk Alzheimer alipofanya uchunguzi katika ubongo wa marehemu na kubaini kuwa kulikuwa na hitilafu katika baadhi ya seli za ubongo wake.

Hivyo, akawa daktari wa kwanza kubaini ugonjwa huo wa kupoteza kumbukumbu na kulifanya Shirika la Afya Duniani (WHO) limpe heshima kwa kuuita ugonjwa huo jina la daktari huyo. Ugonjwa huo unafahamika kama Alzheimer.

Ugonjwa huu ni moja ya matatizo makubwa ya kiafya yanaoikabili dunia hasa katika kipindi hiki ambacho kuna ongezeko la wazee hasa katika nchi zilizoendelea.

Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari, mnamo mwaka 2010 ugonjwa huu ulishika namba ya sita kati ya magonjwa yanayosababisha vifo nchini Marekani.

Ripoti WHO kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Kupambana na Ugonjwa wa Alzheimer (ADI), inakadiria kuwa idadi ya wagonjwa wa tatizo hili itaongezeka mara tatu zaidi ifikapo mwaka 2050 na kuifanya dunia kuwa na wagonjwa zaidi ya milioni 135.

WEWE NI MIONGONI MWA WATU HAO? Siyo jambo la ajabu lakini unapaswa kutunza afya yako.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo kwa sasa kuna watu 44 milioni wanaougua maradhi haya hatari duniani kote. Idadi hii ni sawa na ongezeko la asilimia 22 ya wagonjwa 35.6 milioni waliokuwa na maradhi haya miaka mitatu iliyopita.

Wataalam wanasema, “Ugonjwa huu ni janga la kimataifa na hali inazidi kuwa mbaya. Tunapoangalia hali ya siku za usoni, tunaona kuwa idadi ya wagonjwa itaongezeka sana.” ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu miongoni mwa wazee, ni moja ya magonjwa yanayowakabili watu wenye umri zaidi ya miaka 55 na unasababisha upotevu wa mapato kuliko saratani, kiharusi na magonjwa ya moyo kwa pamoja.

Ugonjwa huu wa wazee, unasababisha mtu kupoteza kumbukumbu ya matukio ya karibuni na kadri ugonjwa unavyoendelea mtu anaweza kushindwa kuzungumza vizuri. Tatizo jingine ni kupoteza uwezo wa kuelewa mazingira anayoishi, kushindwa kujihudumia na kupata mabadiliko ya kitabia kama vile kujitenga na watu wa familia au jamii.

Ingawa hali hii hujitokeza taratibu, lakini inaweza kusababisha kifo ndani ya kipindi cha miaka mitatu hadi tisa. Hii ni kwa mujibu wa utafiti wa S. Todd na wenzake uliochapishwa mwaka 2013 katika jarida la International Geriatric Psychiatry, toleo la 28 (11).

Ingawa chanzo halisi cha maradhi haya hakijulikani bayana, baadhi ya wanasayansi wanaamini kuwa ugonjwa huu unatokana na changamoto za mazingira pamoja na matatizo ya urithi wa vinasaba vya kijenetiki vyenye mwelekeo wa kupata tatizo hili.

Wataalamu wa afya wanaamini chembe za urithi zinachangia kutokea kwa maradhi haya kwa asilimia 70. Katika utafiti wa hivi karibuni uliochapishwa katika jarida la kisayansi la Nature Genetics, ilibainika kuwa kuna takriban aina 20 za vinasaba vya kijenetiki vinavyochangia mtu kupata maradhi haya.

Timu ya watafiti wa taasisi ya Pasteur ya nchini Ufaransa iliyoongozwa na Philippe Amouyel ilipata ushahidi kutoka kwa washiriki wa utafiti zaidi ya 74,000 kutoka nchi 15 sehemu mbalimbali duniani na kubaini kuwa wagonjwa wenye maradhi haya, DNA zao zilikuwa na matatizo yanayofanana.

Mambo mengine yanayotajwa na wanasayansi kuwa yanachangia mtu kupata maradhi haya ni pamoja na shinikizo la damu, msongo wa mawazo pamoja na ajali zinazohusisha kichwa.

Maradhi haya yanaweza kugundulika kwa daktari kuchukua maelezo ya tatizo, historia ya kitabibu, kufanya jaribio la kupima uwezo wa mtu wa kiakili, kupima damu na vipimo vyingine vya uchunguzi kwa kutumia mionzi kama vile MRI.

Kwa ujumla, maradhi haya hayana tiba ya moja kwa moja yanayofanya mgonjwa alirudie hali yake ya kiakili kama awali, ingawa kuna dawa zinazosaidia mtu kukabiliana na dalili za maradhi kama vile msongo wa mawazo.

Mazoezi ya mwili ni muhimu katika programu ya tiba ya wagonjwa wa namna hii ili kuzuia hali isiwe mbaya haraka na kumkinga mgonjwa dhidi ya maradhi yanayowanyemelea watu.

Ulaji wa matunda, mbogamboga, kokwa na nafaka zisizokobolewa pamoja na vyakula vingine ambavyo havijasindikwa, inaweza kuwa njia bora ya kukabili vyanzo vya tatizo hili.


Comments

Popular posts from this blog

Kifafa cha Mimba (Preeclampsia, eclampsia)

MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes Kifafa cha mimba ni ugonjwa unaohusiana na msukumo mkubwa wa damu (high blood pressure) wakati wa ujauzito pamoja na kuharibika kwa viungo muhimu mwilini kama vile figo na ini. Kwa kawaida ugonjwa huu hutokea baada ya nusu ya kwanza ya ujauzito kuisha (kuanzia wiki ya 20 au miezi mitano ya ujauzito). Ugonjwa huu huweza kuwatokea hata wajawazito ambao hawakuwa na tatizo la msukumo mkubwa wa damu kabla ya ujauzito. Ugonjwa wa kifafa cha mimba unaweza kuleta madhara makubwa kwa mjamzito na mtoto aliye tumboni. Kuharibika kwa viungo muhimu kama figo na ini la mjamzito kunaweza kuwa kwa kiwango kikubwa kichoweza kusababisha mjamzito kupoteza maisha iwapo hatapata huduma ya afya mapema. Vilevile mtoto aliye tumboni anaweza kuathirika kwa kukosa damu ya kutosha toka kwa mama na kushindwa kukua vizuri na iwapo hali hiyo ikiendelea muda mrefu anaweza kufia tumboni. Kutokana na hatari kubwa ya ugonjwa huu kwa wajawazito na watoto walio tumboni, ina...

Medical gamble that saved a little boy’s life

  The 18-month old boy was rushed to Muhimbili National Hospital (MNH) in Dar es Salaam where he was admitted. But his condition soon deteriorated into acute kidney failure. A dark cloud hovered over the family. The country’s biggest referral hospital has for years been infamous for being too ill-equipped to save those dying from such conditions. To read the whole story click here

Haya ndiyo madhara ya Kutumia earphones

Imeelezwa kuwa watu wanaotumia redio za simu wako hatarini kupatwa na ugonjwa wa saratani ya sikio na kichwa kutokana na mionzi mikali itokanayo na viselula hivyo. Akizungumza na FICHUO TZ, Dk. Leopard Mwinuka alisema, watakaoathirika na tatizo hilo ni wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikioni ‘headphone’. “Nawaonea huruma wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikio, kwani madhara yake hawawezi kuyaona sasa bali siku zijazo watapata ugonjwa wa saratani,” alisema Dk. Mwinuka. Alimaliza kwa kusema kuwa, mbali na kupata ugonjwa huo, wahusika wanaweza kupata tatizo la kutosikia vizuri kwa sababu, mtu anapotumia spika za sikio huweka sauti kubwa ili apate mdundo mzuri baada ya muda ngoma ya sikio inaathiriwa na hali hiyo. Habari nyingine za kitabibu zilisema kwamba, kwa kuwa pande zote za spika zina sumaku, huweza kuvutana na kuvuruga mpangilio wa ubongo hasa kama spika hizo zitakaa maskioni kwa zaidi ya sa...