Skip to main content

Umuhimu wa Maji mwilini

 
Kunywa maji ni tendo ambalo watu wengi hulifanya pale wanapohisi kiu. Wengine hutumia vinywaji mbalimbali kama vile juisi au soda ili kutuliza kiu. Wataalamu wanashauri matumizi ya maji kwa kutuliza kiu na hata kwa kunywa polepole kwa lengo la kuufanya mwili usikose maji.

Kwa nini maji? Je, yana umuhimu gani katika mwili. 
Umuhimu huo ni miongoni mwa mambo yaliyotiliwa mkazo na madaktari wa binadamu wakati walipokutana na wagonjwa mbalimbali wenye magonjwa sugu.

Mtaalamu wa Magonjwa ya Moyo, wanaelelezea umuhimu wa maji ya kunywa ili kuepuka magonjwa ya moyo.

“Moyo hauwezi kufanya kazi bila maji ambayo ni asilimia 70 ya mwili wa binadamu. Kwa hiyo, unywaji wa maji ni muhimu kwa utendaji wa mwili na hasa zaidi kwa mishipa ya moyo,”

“Nini kinatokea kama mtu hatakunywa maji?
Kwanza, mishipa midogo ya damu katika mwili itafunga. Hii itasababisha upinzani katika mzunguko wa damu na kusababisha kuongezeka kwa shinikizo la damu. Ukosefu wa maji huongeza hatari kwa moyo.”

“Kutumia glasi tano za maji au zaidi kwa siku kwa kiasi kikubwa hupunguza mashambulizi ya moyo kwa kiasi kikubwa, ikilinganishwa na kunywa chini ya glasi mbili za maji kwa siku.”

Zipo faida nyingi za matumizi ya maji iwapo yatatumika kwa kiwango kinachotosheleza. Maji hufanya damu kuwa nyepesi kama inavyotakiwa kuwa, hurahisisha mzunguko wa damu kwenda kwenye moyo, hufanya moyo kutumia nguvu kidogo kusukuma damu na hata kupunguza hatari ya damu kuganda.

Wataalamu wanashauri matumizi ya kubadili tabia kama sehemu ya kukabiliana na maradhi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufuata ushauri wa kitaalamu

Comments

Popular posts from this blog

Kifafa cha Mimba (Preeclampsia, eclampsia)

MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes Kifafa cha mimba ni ugonjwa unaohusiana na msukumo mkubwa wa damu (high blood pressure) wakati wa ujauzito pamoja na kuharibika kwa viungo muhimu mwilini kama vile figo na ini. Kwa kawaida ugonjwa huu hutokea baada ya nusu ya kwanza ya ujauzito kuisha (kuanzia wiki ya 20 au miezi mitano ya ujauzito). Ugonjwa huu huweza kuwatokea hata wajawazito ambao hawakuwa na tatizo la msukumo mkubwa wa damu kabla ya ujauzito. Ugonjwa wa kifafa cha mimba unaweza kuleta madhara makubwa kwa mjamzito na mtoto aliye tumboni. Kuharibika kwa viungo muhimu kama figo na ini la mjamzito kunaweza kuwa kwa kiwango kikubwa kichoweza kusababisha mjamzito kupoteza maisha iwapo hatapata huduma ya afya mapema. Vilevile mtoto aliye tumboni anaweza kuathirika kwa kukosa damu ya kutosha toka kwa mama na kushindwa kukua vizuri na iwapo hali hiyo ikiendelea muda mrefu anaweza kufia tumboni. Kutokana na hatari kubwa ya ugonjwa huu kwa wajawazito na watoto walio tumboni, ina...

Medical gamble that saved a little boy’s life

  The 18-month old boy was rushed to Muhimbili National Hospital (MNH) in Dar es Salaam where he was admitted. But his condition soon deteriorated into acute kidney failure. A dark cloud hovered over the family. The country’s biggest referral hospital has for years been infamous for being too ill-equipped to save those dying from such conditions. To read the whole story click here

Haya ndiyo madhara ya Kutumia earphones

Imeelezwa kuwa watu wanaotumia redio za simu wako hatarini kupatwa na ugonjwa wa saratani ya sikio na kichwa kutokana na mionzi mikali itokanayo na viselula hivyo. Akizungumza na FICHUO TZ, Dk. Leopard Mwinuka alisema, watakaoathirika na tatizo hilo ni wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikioni ‘headphone’. “Nawaonea huruma wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikio, kwani madhara yake hawawezi kuyaona sasa bali siku zijazo watapata ugonjwa wa saratani,” alisema Dk. Mwinuka. Alimaliza kwa kusema kuwa, mbali na kupata ugonjwa huo, wahusika wanaweza kupata tatizo la kutosikia vizuri kwa sababu, mtu anapotumia spika za sikio huweka sauti kubwa ili apate mdundo mzuri baada ya muda ngoma ya sikio inaathiriwa na hali hiyo. Habari nyingine za kitabibu zilisema kwamba, kwa kuwa pande zote za spika zina sumaku, huweza kuvutana na kuvuruga mpangilio wa ubongo hasa kama spika hizo zitakaa maskioni kwa zaidi ya sa...