Skip to main content

Posts

Showing posts from July, 2016

Lowassa ampongeza Rais Magufuli kwa utendaji kazi

MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa amempongeza Rais John Magufuli kwa utendaji wake tangu ashike nafasi ya urais Novemba mwaka jana. Hata hivyo, Waziri Mkuu huyo wa zamani amebainisha kuwa ingekuwa ni yeye amepata nafasi ya urais, angeanza na vipaumbele vyake ambavyo ni ajira na maslahi ya walimu ili kuboresha zaidi maeneo hayo. Lowassa aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akihojiwa na mtangazaji Tido Mhando kwenye kipindi cha Funguka, kinachorushwa na Televisheni ya Azam. Alikiri kuwa Dk Magufuli hadi sasa ameonekana kufanya vizuri katika utendaji wake, ikiwemo suala la ufisadi na hatua yake ya kutekeleza kwa vitendo kuhamishia serikali mkoani Dodoma. “Amefanya kazi nzuri katika maeneo fulani, amefanya vizuri sana. Kuna maeneo amesema mwalimu unaweza kufagia shilingi, na yeye amefagia shilingi. Ila kuuna maeneo kwa maoni yangu ningeyapa kipaumbele zaidi kwa mfano ajira,” alisisitiza. ...

WANANCHI WA KIJIJI CHA ILININDA WILAYANI LUDEWA WACHANGISHANA PESA MIFUKONI MWAO ILI KUKARABATI BARABARA

MTU KWAO/ Eagle Eyes WANANCHI WA KIJIJI CHA ILININDA WILAYANI LUDEWA WACHANGISHANA PESA MIFUKONI MWAO ILI KUKARABATI BARABARA,  Na Maiko Luoga Ludewa, Barabara ya Kutoka Kijiji cha ilawa Hadi Ilininda wilayani Ludewa imedumu kwa Muda mrefu ikiwa mbovu bila matengenezo Hatimaye Wananchi Wa Kijiji cha Ilininda kwakushirikiana na Wadau mbalimbali ndani ya Kata ya Madilu Wilayani Ludewa katika Mkoa Wa Njombe wameamua Kuingia Mifukoni mwao na Kuchangishana Pesa kwa Umoja wao ili kuikarabati barabara hiyo Bila kuisubiri Serikali. Wakizungumza na Mwandishi wetu wananchi Wa Kijiji cha Ilininda wamesema Baada ya Kuona barabara yao Ipo katika hali mbaya wameweza kushirikiana na Uongozi Wa NGO ya IDEFO hadi kuchangia kiasi cha Sh. 15 million Ambazo tayari zimetumika Kulipia mafuta Kwa mtu aliyewasaidia kupata Mashine na Uchimbaji Wa Barabara hiyo unaendelea Huku wakiiomba Serikali kuwasaidia Pesa kwaajili ya Kuendelea Kuikarabati barabara hiyo waliyoamua kuichimba kwa Nguvu zao wenyew...

Waislamu wajiunga na wakatoliki katika ibada

MTU KWAO/ Eagle Eyes Waislamu wajiunga na wakatoliki katika ibada WaIslamu zaidi ya mia moja wamejumuka na Wakatoliki katika sala iliyohudhuriwa na waumini wengi katika Kanisa moja huko Rouen, Ufaransa. Tukio hilo limewadia , siku tano baada ya kasisi wa kanisa hilo , kuuawa na wapiganaji wa Kiislamu. Muungano huo unalenga kuonesha umoja dhidi ya mauaji ya kasisi Makanisa sehemu mbali mbali za Ufaransa, yaliwaalika WaIslamu wajumike nao kwenye maombi leo, kuonesha wanakanusha mauaji hayo. Mauaji ya hivi karibu kabisa yaliyotekelezwa na wapiganaji wa Kiislamu, yameshtua Ufaransa. Kasisi huyo wa umri wa miaka 86, Kasisi Jacques Hamel, aliuwawa akiwa kwenye maombi.

Download Kalajeremiah fr Miriam marwa_Wana ndoto

  Kala jeremiah katoa ngoma mpya akishirikia na Miriam marwa . Ngoma inakwenda kwa jina la WANA NDOTO. Click here to Download

MAGUFULI ATENGUA UTEUZI MWINGINE LEO

Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi iliyotolewa leo July 28 2016 mjini Dodoma imeeleza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Barabara (Road Fund Board) Dkt. James Munanka Wanyancha. Rais Magufuli ametengua uteuzi huo kuanzia leo July  28 2016. Kufuatia kutenguliwa kwa uteuzi huo, Rais Magufuli amemteua Joseph Odo Haule kuwa Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Mfuko wa Barabara. Uteuzi wa Joseph Odo Haule umeanza leo July 28 2016. Kabla ya uteuzi huo Joseph Odo Haule alikuwa Meneja wa Mfuko wa Barabara (Road Fund). Wajumbe wengine wa Bodi ya Mfuko wa Barabara wanaendelea katika nafasi zao.

Papa Francis Aanguka Ghafla Akiongoza Misa

Latest 08:31 AM Mrembo Tunda Afunguka Kumwagana na Mwanamuziki Young D 343 ONLINE Home » »Unlabelled » Papa Francis Aanguka Ghafla Akiongoza Misa Papa Francis Aanguka Ghafla Akiongoza Misa POLAND: Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis, ameanguka ghafla wakati akiwa anaongoza misa, baada ya kujisikia vibaya. Inadaiwa Papa husumbuliwa na tatizo la maumivu ya miguu na mgongo

Ajuza wa miaka 89 abakwa na kuuawa

MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes CHRISTINA Mnyira (89) mkazi wa Patandi wilayani Arumeru mkoani Arusha amekutwa amekufa baada ya kubakwa na kunyongwa shingo. Mnyira alikutwa amekufa Julai 21 mwaka huu. Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Arusha, Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha, Yusuph Ilembo alisema kijana mmoja ametiwa mbaroni na mwingine anasakwa. Alisema baada ya bibi huyo kufanyiwa unyama huo mwili wake ulitupwa katika msitu wa Chuo cha Mifugo Tengeru na wasamaria wema walitoa taarifa polisi.

MAUMIVU YA TUMBO WAKATI WA HEDHI

MTU KWAO BLOG / Eagle eyes KARIBU sana katika makala yetu inayohusu afya.Kutokana na simu nyingi ninazozipata nikiulizwa maswali juu ya maumivu yanayowapata akina mama wengi wakati wa hedhi nimeona ni bora niandike makala hii ili iweze kuwasaidia na wengine kujua nini chanzo na mhusika afanye nini pale anapopatwa na tatizo hilo. Maumivu wakati wa hedhi (period pains) au kitaalamu dismenorrhea, ni maumivu yanayojitokeza sehemu ya chini ya tumbo au kiunoni wakati mwanamke anapoanza kupata siku zake au kabla ya hapo. Maumivu hayo huweza kuwa madogo au ya wastani huku baadhi ya wanawake wakipata maumivu makali sana. Maumivu hayo huanza pale yai linapotoka katika mrija (fallopian tube) na kuteremka chini ya mrija huo wakati wa Ovulation. AINA YA MAUMIVU Maumivu ya tumbo la hedhi yapo ya aina mbili.   Ya kwanza ;  ni maumivu yasiyokuwa na sababu zozote za kimsingi za kitiba. Katika aina hii maumivu ni ya kawaida na huhisiwa sehemu ya chini ya tumbo na kiunon...

KUTIZAMA TV KUNAHATARISHA AFYA YAKO

MTU KWAO BLOG /Eagle Eyes  Utafiti uliofanywa na wanasayansi wa Japan umethibitisha kwamba kukaa kwa mda mrefu na kutazama vipindi vya televisheni kwa masaa mengi kunahatarisha afya kwani huhusishwa na maradhi yanasababisha mzunguko wa damu mwilini kutokuwa sawa. Watafiti hao wanasema, hali hiyo pia huenda ikasababisha damu kuganda na kutengeneza vidonge katika sehemu kama vile miguu, na iwapo mgando huo utasukumwa na nguvu za mzunguko wa damu na kuingia sehemu kama vile mapafu, husababisha vifo. Utafiti huo ulihusiha watu zaidi ya 86,000 ambao hupendelea kutazama televisheni katika mida mbalimbali kwa siku. Kisha afya zao zilifuatiliwa kwa zaidi ya miaka 19 tangu mwaka 1988 hadi 1990. Matokeo yalikuwa kila muda wa masaa mawili yalipopita mtu akikaa kutazama televisheni, nayo hatari ya kupata ugonjwa huo wa mapafu uitwao ‘Fatal pulmonary embolism’ ulioongezeka kwa asilimia 40%. Iligundulika pia kuwa waliotazama vipindi vya televisheni kwa zaidi ya saa 5 walik...

MSANII WA BONGO NAY WA MITEGO AFUNGIWA KUIMBA

Baraza la sanaa la taifa ( BASATA) limemfungia kwa kipindi kisicho julikana msanii Wa mziki Wa kizazi kipya Emmanuel Elibariki maarufu kwa jina LA ney Nay WA Mitego hadi hapo litakapo jiridhisha kwamba ametekeleza maagizo yote aliyopewa na Baraza sambamba na yeye kibadilika katika kubuni kazi zenye maadili na zisizo dhalilisha watu Wa kada mbalimbali.

Download Prof Jay ft Shalo Mwamba

Proffesor Jay ft Shalo mwamba hii hapa ngoma yao mpya inaitwa Kazi kazi. Kama ulikuwa bdo hujapakua ipakue  hapa sas DOWNLOAD HERE

ALICHOKISEMA YUDA KUHUSU UNSATA

Aliyekuwa Mhasibu wa UNSATA Yuda Lulay amezungumza na baadhi ya wanachama wa unsata. ➡A kizungumzia kuhusu suala katiba na kuvunja muungano kati ya Bachelor na Diploma.  Raisi wa UNSATA ndiye kikwazo kikubwa . Pia ameshangazwa na suala la uchaguzi linaloendelea chini ya karpet . ➡wew kama mwana UNSATA unamaoni gani . ✅DR FOC

Koffi Olomide ahukumiwa kifungo cha mwaka 1

Mwanamuziki nguli wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Koffi Olomide amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela huko DRC kwa kumpiga teke mmoja wa madansa wake aitwaye Pamela akiwa nchini Kenya. Nguli huyo wa muziki wa Rhumba amehukumiwa muda mfupi baada ya kukamatwa na polisi akiwa nyumbani kwake mjini Kinshasa leo. Koffi alikana tuhuma za kumpiga dansa huyo na mwanasheria wake aitwaye George Wajackoyah naye amelaani kitendo cha polisi kutumia nguvu kubwa wakati wa kumkamata staa huyo. VIDEO: Koffi Olomide adaiwa kumpiga teke mwanamke Kenya bofya hapa Staa huyo alikamatwa nchini Kenya Ijumaa iliyopita na kurudishwa DRC kesho yake asubuhi baada ya video yake kusambaa mitandaoni ikimuonesha akimpiga teke mmoja wa madansa wake aitwaye Pamela mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Jomo Kenyatta (JKIA) kwa ajili ya tamasha. Koffi anadaiwa kufanya tukio hilo baada ya Pamela kukorofishana na mwanamuziki wake aitwaye Cindy Le Couer anayedaiwa kuwa ni mpenzi wa K...

MIGRAINE HEADACHE .@Kipanda uso na tiba yake

MTU KWAO BLOG /01 DALILI ZA KIPANDA USO Kipanda uso (Migraine) ni ugonjwa au maumivu makali ya kichwa anayokuwa nayo mtu baada ya mshipa wa damu (Enlargement of Artery ) kutanuka katika kichwa chake. Baada ya kutanuka kwa mishipa hii ya damu, pia kuna kemikali ndani ya mwili zinazozalishwa na kuizunguka mishipa hii na kupelekea mtu apate maumivu makali ya kichwa na kutanuka zaidi kwa mishipa.Maumivu makali ya kichwa hupelekea mfumo wa utendaji kazi wa mwili pia ubadilike, mtu atapatwa na kichefuchefu, kutapika, kuharisha, katika utumbo chakula hakitanyonywa vizuri kiingie mwilini, mtu atashindwa kuona vizuri maeneo yenye mwanga na kutopenda kukaa mazingira yenye sauti au kelele. Vipo vitu mbalimbali vinavyoweza kuchangia mtu apate tatizo la kipanda uso,  vitu hivi haimaanishi kuwa ni lazima vikusababishe upate na hata kama haupo katika mazingira ya vitu hivi haimaanishi kuwa huwezi kupata tatizo la kipanda uso, miongoni mwa vitu hivyo ni kama vile:  sauti...

NJIA 3 ZA ASILI ZA KUONDOA WEUSI KATIKA MAPAJA NA MAKWAPA

MTU KWAO BLOG /01 Inner thighs/mapaja ya ndani na makwapa hutokea weusi kutokana na msuguano wa ngozi kwasababu ya mapaja kugusana, hata ngozi iliyokauka pia inaleta weusi katika ngozi. Hivyo nimekuletea njia natural ya kuondoa weusi huo bila kutumia madawa makali. 1.TUMIA MAFUTA YA NAZI NA NDIMU. Mafuta ya nazi yanatumikakulainisha ngozi lakini unaweza kutumia pia katika kuondoa weusi ukichanyanya na ndimu..fata step hizi:: Chukua vijiko 3 vya mafuta ya nazi changanya na ndimu nusuPaka sehemu yenye weusi katika mapaja huku ukisugua kama unafanya massage kwa dakika 15.Kisha osha na maji ya uvuguvugu na kausha kwa kitambaa kilaini na kisafi. 2.TUMIA MCHANGANYIKO WA SUKARI ASALI NA NDIMU. Mchanganyiko huu pia unaweza ukaondoa weusi katika mapaja na makwapa, fuata step hizi:: Changanya kijiko kimoja cha asali, ndimu nusu na kijiko kimoja cha sukari.Paka sehemu yenye weusi na sugua kawaida hadi sukari ipotee.Acha ikae kama dakika 10 kisha osha na maji ya uvuguvugu. ...

Ommy Dimpoz amwagana na meneja wake Mubenga

MTU KWAO BLOG /01 Mubenga na Ommy Dimpoz Aliyekuwa meneja wa PKP ya Ommy Dimpoz, Mubenga, amesema hafanyi tena kazi na muimbaji huyo wa wimbo ‘Achia Boby’ huku akiweka wazi mpango wa kuanzisha label yake mpya. Mubenga ambaye alifanya kazi kwa muda mrefu na Ommy Dimpoz amekiambia kipindi cha Enewz cha EATV kuwa ameakua kuachana na PKP ili afanye mambo yake mengine. “Kwa sasa najipanga ili kuja na kampuni yangu ambayo itaitwa Bengaz Entertainment ambayo itakuwa inahusika na maswala yote ya burudani, hivyo wadau wangu waelewe kwamba kwa sasa sifanyi kazi tena na pozi kwa pozi”. Hata hivyo Mubenga hakuweka wazi sababu iliyopelekea yeye kuachana na PKP huku akisisitiza kuwa anarudi katika kazi zake alizokuwa akizifanya kabla ya kuungana na pozi kwa pozi.

Mvua ya samaki ilivyotingisha Thailand

MTU KWAO BLOG /01 Hebu vuta picha, umeamka asubuhi na kuingia barabarani kwa ajili ya kuelekea eneo lako la kazi ghafla unakutana na samaki wengi wakiwa wametapakaa kwenye lami, huku watu wakieleza kwamba samaki hao wamedondoka kutoka angani kufuatia mvua kubwa iliyonyesha usiku! Ni jambo la ajabu si ndiyo? Basi kwa taarifa yako, tukio kama hilo limewahi kutokea nchini Thailand. Aprili 16, 2015, wananchi wa Thailand walishuhudia tukio la ajabu la maelfu ya samaki kukutwa barabarani, huku ikielezwa walishuka na mvua iliyonyesha usiku kucha. Habari hiyo ilisambaa kwa kasi ikisindikizwa na picha zilizokuwa zinaonesha barabara ya lami ikiwa imefurika samaki hao. Hata hivyo, baada ya taarifa hizo kuwa zimesambaa kwa kasi ya ajabu na kuzua mshangao karibu dunia nzima, baadaye ilibainika kwamba samaki hao hawakuwa wameshuka na mvua kutoka angani. Taarifa kutoka kwenye mamlaka zinazohusika, zilieleza kwamba samaki hao walitapakaa barabarani baada ya lori kubwa lililokuwa lime...

Diwani Akwepa Risasi sita akipambana na majambazi Moshi

MTU KWAO BLOG /01 Diwani  wa Kata ya Kiborlon (Chadema) katika Manispaa ya Moshi, Frank Kagoma ameonyesha ujasiri wa hali ya juu alipopambana na majambazi waliokuwa na silaha za moto.  Alinusurika kuuawa baada ya majambazi hao waliokuwa na bunduki na bastola kumfyatulia risasi sita alipokuwa akiwafukuza ambazo hata hivyo, hazikumpata. Tukio hilo ambalo lilionekana kama sinema, lilitokea mwishoni mwa wiki baada ya majambazi hao kuvamia duka la jumla la kuuza mitumba linalomilikiwa na Menti Mbowe na kupora Sh10 milioni. Katika tukio hilo lililotokea saa tano asubuhi eneo la Kiborlon, majambazi hao walimjeruhi kichwani mfanyabiashara huyo anayemiliki pia mabasi ya Machame Safaris. Hali ya majeruhi huyo inaendelea vizuri. Akisimulia tukio hilo, diwani huyo alisema siku hiyo akiwa maeneo ya Kiborlon, alipigiwa simu kuwa mfanyabiashara huyo amevamiwa na majambazi ndipo alipoendesha gari lake hadi eneo la tukio. “Nilipofika pale wale majambazi watatu ndiyo walikuw...

Unyonyaji kidole unafaida kwa watoto- Utafiti

MTU KWAO BLOG/01 Image copyrightTHINKSTOCKImage captionUnyonyaji kidole unafaida kwa watoto- Utafiti Ripoti mpya inasema watoto wanaonyonya vidole au kung'ata kucha zao kwa meno huenda wasipate matatizo ya kuathirika kutokana na mazingira hewa au kula vyakula fulani. Kwa mujibu wa waandishi katika jarida la Pediatrics, huo ni ni usafi dhanio,kwani yatokanayo na baadhi ya wadudu huimarisha mfumo wa kinga ya mwili. Unyonyaji wa kidole gumba na ung’ataji wa kucha umeonekana kuzuia baadhi ya alergy. Kati ya watu elfu moja wenye umri wa kati ya miaka mitano hadi thelathini na mbili,walifanyiwa uchunguzi kwa muda nchini New Zealand. Lakini tabia hii ya unyonyaji vidole na ung’ataji kucha haisaidii watu wenye pumu au mtu anapopata homa kali. Uchunguzi uliofanywa na kurekodiwa kwa watoto wenye umri wa kati ya miaka mitano na kumi na moja na wengine waliofanyiwa vipimo ni wenye umri kati ya miaka kumi na tatu na thelathini na miwili. Huku thuluthi moja ya watoto hao ni wanyo...

UGONJWA WA MAFINDOFINDO (TONSILS)

MTU KWAO BLOG /01 Tonsil husababishwa na sababu nyingi tu . Pia husababishwa na upungufu wa white blood Cells katika mwili ambazo cells hizi ndio hupigana na vidudu vyote venye kuleta maradhi ndani ya mwili sasa vinaposhindwa kufanya kazi lymph zinavimba na husababisha Tonsils. Kila mtu na ukuwaji wake wa mwili, wapo ambao wanapata tonsils kwa kunywa maji ya baridi ambayo maji ya baridi huwa ni moja katika chanzo cha kupata tonsils, mavumbi huchangia vile vile pilipili na vitu vikali kama vile embe mbichi limau pia huwa ni sababu kuu ya kupata tonsil. Wakati unapokuwa na tonsils muhimu zaidi kuacha maji ya baridi na vitu vyote vikali, zaidi utumie maji ya moto Dawa za tonsils ni : kama ni mtumiaji wa dawa za chemicals basi epincilin inasaidia sana kuondosha tonsils. Dawa nyengine ambayo mimi binafsi naipendelea hii zaidi kwani inafanya kazi mara moja : Kamua ndimu moja katika glass yako kisha tia maji ya Uvuguvugu (warm water) na baadae tia vijiko vinne vidogo vya asal...

FAHAMU FAIDA ZA KUNYWA GREEN JUICE KWA MWILI NA AFYA.

MTU KWAO BLOG /01 Good morning Loves, so kwa wale watu wa fitness na wanaopenda to keep their bodies healthy nadhani mtakuwa mnajua green juice ni nini na jinsi ya kuitengeneza and all that. Since I spend most of my time reading and writing nimekutana na sehemu mtu anauliza hii green juice inasaidia nini haswa, yaani faida zake ni nini, kwanini unywe green juice? Kwanini unywe Green Juice? 1.Inasafisha ngozi yako. Baada ya kama wiki mbili za kunywa green juice utaanza kuona mabadiliko, ngozi yako itaanza kuwa laini na hata madoa na makovu uliyokuwa nayo yataanza kupotea. If you make a habit ya kuinywa kila siku basi ngozi yako ndio itatakata kabisa. 2.Inakupa nguvu. Kwa wale ambao tayari mnakunywa green juice mtakuwa mnajua kuwa unatakiwa kuinywa on ana empty stomach.. kunywa ukiwa huna kitu tumboni, kaa kama nusu saa ndio unaweza kunywa au kula kitu kingine. Green juice ina nutrients nyingi na hivyo ni bora kama ukiinywa asubuhi kabla hujala kitu kingine chochote. 3.Inasa...

Ndege inayotumia jua kukamilisha safari yake

MTU KWAO BLOG /01  Ndege inayotumia nguvu ya miale ya jua imeondoka mjini Cairo nchini Misri kwenda Abu Dhai katika awamu yake ya mwisho ya safari ya kuizunguka dunia. Ndege hiyo inayofahamika kama Solar Impulse 2, ilianza safari yake mjini Abu Dhabi mwezi Machi mwaka 2015. Akiongea na BBC, akiwa katika anga za bahari ya shamu , rubani wa ndege hiyo Bertrand Piccard, amesema kuwa ana matumaini kuwa ndege zinazotumia miale ya jua zinaweza kuwasafirisha hadi abiria 50 ndani ya kipindi cha miaka kumi. Amesema kuwa teknolojia mpya anayoifanyia majaribio inaweza kusaidia kupunguza kwa nusu mafuta inayotumiwa kila siku.

Mchungaji Feki na Waumini wawekwa Mikononi mwa Polisi DSM

Anayejiita mchungaji David Mwamkinga amejikuta mikononi mwa polisi jijini Dar es Salaam baada ya ndugu wa baadhi ya wafuasi wa mchungaji huyo kuamua kuwatoa ndugu zao waliofungiwa ndani kwa zaidi ya miaka 10 , kwa lengo la kufanyiwa maombi kutokana na maradhi yanawasumbua. Hatua hiyo inafuatia kilichoelezewa kuwa ni kuzidi kudhoofika kwa hali za waombewaji hao ambapo jeshi la polisi limeingilia kati na kufanikiwa kumkamata mchungaji huyo pamoja na wafuasi wake eneo la Magomeni Kagera na kuelekea nao kituoni.

Vinara wa Lugha Chafu Kwa Wagonjwa Bariadi Kuwajibishwa

Kufuatia malalamiko ya wananchi ya muda mrefu kuhusiana na kukithiri kwa zisizofaa kwa wagonjwa zinazotolewa  na baadhi ya watumishi wa idara ya afya katika hospitali ya Somanda halmashauri ya mji wa bariadi, mganga mkuu ameagizwa kuwawajibisha  wanaodaiwa kuwa vinara wa lugha hizo pamoja na wale wasiozingatia maadili ya utumishi wao. Agizo hilo limetolewa na mkuu wa wilaya ya Bariadi festo kiswaga alipokutana na watumishi wa afya hospitalini hapo katika kikao cha pamoja ili kuwakumbusha wajibu na majukumu yao wanayopaswa kuyatekeleza wakiwa katika maeneo yao ya kazi ambapo  amesema ni lazima wawajibishwa wenye tabia hizo kwani kauli chafu dhidi ya wagonjwa zinawasababishia maumivu Zaidi wagonjwa . Katika hatua nyingine ametoa wiki moja kuhakikisha hospitali hiyo iliyokithiri kwa uchafu ,mazingira yake yawe katika hali ya usafi ,ili kuepuka magonjwa ya milipuko. Kwa upande wake mganga mkuu wa  halmashauri ya mji wa bariadi dkt akilimali mpozemenya  ames...

Polisi wamsaka daktari feki aliyesababisha kifo

POLISI mkoani Singida inamtafuta mtu mmoja aliyewahi kuwa Mganga Msaidizi Vijijini (RMA) kwa tuhuma za kusababisha kifo cha mzee wa miaka 70 baada ya kumfanyia upasuaji wa tezi dume. Inadaiwa kuwa RMA huyo ambaye alikuwa mwajiriwa serikalini miaka mingi iliyopita, alifanya upasuaji huo Julai 14 mwaka huu akiwa hana ujuzi, utaalamu wala vifaa vya kufanyia shughuli hiyo. Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi mkoa wa Singida, Thobias Sedoyeka, mtuhumiwa huyo Joseph Msafiri (40) ni mkazi wa Kijiji cha Kinyambuli, wilayani Mkalama mkoani hapa ambaye alimfanyia upasuaji Israel Shaban (68) mkazi wa kijijini hapo. Mtuhumiwa huyo anayedaiwa kugeuza nyumba yake kuwa kituo cha kutolea huduma za afya, alimchukua mzee huyo hadi nyumbani kwake kisha akamfanyia upasuaji wa tezi dume, hata hivyo mzee huyo alipoteza maisha muda mfupi baada ya kutokwa damu nyingi. Kamanda Sedoyeka alisema kuwa baada ya mtuhumiwa kuona hivyo, alitoroka na kutokomea kusikojulikana.

Rais Mafuguli, haya ndio matarajio

Dar/ Mikoani.  Siku moja kabla ya Rais John Magufuli kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, wenyeviti na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wamemtaka kufanya mabadiliko makubwa ya kukisaficha chama. Kikao hicho jana kilipitisha jina la Rais Magufuli kuwa mgombea pekee wa nafasi ya Mwenyekiti wa CCM katika uchaguzi utakaofanyika leo, kwa mujibu wa msemaji wa chama hicho, Christopher ole Sendeka. Makada walioulizwa na Mwananchi swali la ‘Wanataka Magufuli aifanyie nini CCM’, wengi wamemtaka aondoe makundi yaliyopo kwenye chama, huku baadhi wakitaka akisafishe kwa kushughulikia mafisadi na watendaji wasio waaminifu.

DC Aagiza Mganga Kusimamishwa Kazi Geita

DC Aagiza Mganga Kusimamishwa Kazi Geita MKUU wa wilaya Geita Hermani Kapufi , amemwagiza mkurugenzi wa halmashauri ya Geita Alli Kidwaka kumuondoa mara moja mganga wa Zahanati ya Karoro wilaya na mkoa wa Geita Daniel Zengo , kwa madai ya kuuza dawa za Serikali kwenye duka lake binafsi. Amesema hayo wakati akizungumza na mamia ya wananchi kwenye mkutano wa hadhara ulifanyika kwenye Stand mjini Katoro lengo likiwa ni kujadili shughuli za maendeleo na kusikiliza kero za wananchi. Kapufi amesema kuwa mganga huyo anatakiwa kuondoka kwenye kituo hicho na kufunga duka lake mara moja huku akiagiza kamati ya ulinzi na usalama kufuatilia. Naye mganga mkuu wa Hospitali ya wilaya ya Geita amekili kuwepo kwa changamoto hizo na kuahidi kunza kuzitatua

Vijue Vyakula Hatari kwa Kupunguza Nguvu za Kiume

Vijue Vyakula Hatari kwa Kupunguza Nguvu za Kiume Mbegu za Flax (Flax seeds):   Wanaume wanapaswa kufahamu aina ya vyakula ambavyo si rafiki kwao katika kuongeza kiwango cha homoni ya kiume iitwayo testosterone inayochochea sifa ya mwanaume yaani kuwa na nguvu za kiume. Baadhi ya vyakula visivyofaa kuliwa na mwanaume aliyetaka kuwa na nguvu za kiume ni vile vyenye asili ya homoni ya kike iitwayo estrogen. Hivyo sio kila vyakula vinafaa kwa mwanaume eti ilimradi tu vyakula hivyo vinasaidia kujenga mwili au kujaza tumbo wakati mtu akiwa na njaa. Vyakula visivyofaa kabisa kuliwa na mwanaume kutokana na vyakula hivyo kupunguza homoni ya testosterone ni hivi vifuatavyo: vyakula vinavyotengenezwa kutokana na unga wa mbegu za flax vimekuwa vikisifiwa kwa kuwa Omega-3 fats ambayo ni muhimu katika miili yetu. Hata hivyo mbegu za flax ni mbegu maarufu kwa kuwa na estrogen ambayo ni sawa kabisa na homoni ya estrogen iliyoko katika miili ya wanawake. Flax seeds zina kiwango ch...

Darassa - Too Much ( Official Music Video)

Uchawi wa kizungu balaaaaa

Best dancer on the world

USHAURI KWA WANAFUNZI WANAOTARAJIA KUOMBA VYUO VIKUU KUPITIA TCU 2016/2017

USHAURI KWA WANAFUNZI WANAOTARAJIA KUOMBA VYUO VIKUU KUPITIA TCU 2016/2017 Nachukua nafasi hii kuandika makala hii kuweza kutoa ushauri na kuweza kuwaeleza machache niyajuayo katika sakata zima la uombaji wa vyuo vikuu kupitia  TCU. Uombaji wa chuo ni swala nyeti ambalo linahitaji umakini na ushaur chanya kuweza kukamilisha mchakato huo kikamilifu.Yafuatayo ni mambo ambayo unapaswa kuzingatia katika uchaguzi wa chuo na fani tahasusi. 1) MATOKEO YAKO NDIO KIGEZO CHAKO:    Jambo la msingi kabisa ni kujitathmini kua kutokana na matokeo yangu haya naweza kusomea fani gani,na chuo gani ili kuweza kufikisha malengo yangu.Katika nukta hii napenda nigusie vitu vifuatavyo kwa ufupi kabisa.          I.            Kwanza,nikupitia vizuri muongozo wa kitabu cha TCU,Hapo utapata kuoana orodha ya vyuo tafauti ,fani ,minimum entry requirements pamoja na gharama ya chuo ...

APPLICATION ZA MASOMO KOZI MBALIMBALI CHUO CHA DIT 2016/2017

For All wishing to apply for Diploma Courses at DIT. Applications is now open. Click here to start. Application Procedures Step One :: Read Application Requirements Before starting registration. read DIT Admission Requirements Dit Bank Account No: 0150408417800 - CRDB BANK, Account name DSM INST OF TECHNOLOGY 1. Prepare a list of Scanned documents for Attachments All Applicants must have Recent Digital or Scanned Passport size Photo (Scanned passport size photo must single and in full page) Scanned original Birth Certificate . Scanned original Bank Payin Slip. Applicants with O-Level (CSEE from NECTA) only Scanned original O-Level education Certificate (CSEE). Applicants with A-Level (CSEE and ACSEE from NECTA) Scanned original O-Level education Certificate (CSEE). Scanned original A-Level education Certificate (ACSEE) . Applicants with VETA and CSEE from NECTA Scanned original O-Level education Certificate (CSEE). Scanned original VETA Certificate (VETA). Applicants with educ...

ZARI AKANA KUWA NA MTOTO MKUBWA WA KIKE

Taarifa zimesambaa mtandaoni kuwa mpenzi wa msanii, Diamond Platnumz, ambaye amezaa naye mtoto mmoja, Tiffa,Zari kuwa ana mtoto mkubwa aitwaye Zuleha ambaye amekuwa akimficha na kumtambulisha mbele za watu kuwa ni mdogo wake, Zari amekanusha taarifa hizo. ‘’Mimi mbona sina mtoto mwingine wa kike zaidi ya Tiffah tu, achana na ambao hawana akili wavuta bangi, wanatafuta kiki, hasira zao wananitolea mimi, anahangaika na maisha, nina watoto watatu wa kiume na mmoja wa kike na kila mtu anawafahamu hayo mambo mengine siyajui" Alisema Zari.

DIAMOND AACHIA NGOMA MPYA DOWNLOAD HAPA

Mwanamziki wa bongo flava Diamond chibu Dangote ameachia ngoma yake mpya ipakue hapa inaitwa I LOVE YOU DOWNLOAD