Skip to main content

Mvua ya samaki ilivyotingisha Thailand


MTU KWAO BLOG /01
Hebu vuta picha, umeamka asubuhi na kuingia barabarani kwa ajili ya kuelekea eneo lako la kazi ghafla unakutana na samaki wengi wakiwa wametapakaa kwenye lami, huku watu wakieleza kwamba samaki hao wamedondoka kutoka angani kufuatia mvua kubwa iliyonyesha usiku!
Ni jambo la ajabu si ndiyo?
Basi kwa taarifa yako, tukio kama hilo limewahi kutokea nchini Thailand. Aprili 16, 2015, wananchi wa Thailand walishuhudia tukio la ajabu la maelfu ya samaki kukutwa barabarani, huku ikielezwa walishuka na mvua iliyonyesha usiku kucha.
Habari hiyo ilisambaa kwa kasi ikisindikizwa na picha zilizokuwa zinaonesha barabara ya lami ikiwa imefurika samaki hao.
Hata hivyo, baada ya taarifa hizo kuwa zimesambaa kwa kasi ya ajabu na kuzua mshangao karibu dunia nzima, baadaye ilibainika kwamba samaki hao hawakuwa wameshuka na mvua kutoka angani.
Taarifa kutoka kwenye mamlaka zinazohusika, zilieleza kwamba samaki hao walitapakaa barabarani baada ya lori kubwa lililokuwa limebeba shehena ya samaki hao, likielekea kwenye Mji wa Guizhou Kaili, kupata hitilafu kwenye milango yake.
Taarifa ilieleza kwamba mlango wa nyuma ulifunguka bila dereva kujua, samaki wakawa wanadondoka barabarani kwa wingi ndipo watu wakazusha kwamba waliletwa na mvua kubwa iliyonyesha usiku,” ilikaririwa taarifa kutoka kwenye mamlaka zinazohusika nchini humo na kumaliza utata kuhusu ‘mvua ya samaki’.

Comments

Popular posts from this blog

Kifafa cha Mimba (Preeclampsia, eclampsia)

MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes Kifafa cha mimba ni ugonjwa unaohusiana na msukumo mkubwa wa damu (high blood pressure) wakati wa ujauzito pamoja na kuharibika kwa viungo muhimu mwilini kama vile figo na ini. Kwa kawaida ugonjwa huu hutokea baada ya nusu ya kwanza ya ujauzito kuisha (kuanzia wiki ya 20 au miezi mitano ya ujauzito). Ugonjwa huu huweza kuwatokea hata wajawazito ambao hawakuwa na tatizo la msukumo mkubwa wa damu kabla ya ujauzito. Ugonjwa wa kifafa cha mimba unaweza kuleta madhara makubwa kwa mjamzito na mtoto aliye tumboni. Kuharibika kwa viungo muhimu kama figo na ini la mjamzito kunaweza kuwa kwa kiwango kikubwa kichoweza kusababisha mjamzito kupoteza maisha iwapo hatapata huduma ya afya mapema. Vilevile mtoto aliye tumboni anaweza kuathirika kwa kukosa damu ya kutosha toka kwa mama na kushindwa kukua vizuri na iwapo hali hiyo ikiendelea muda mrefu anaweza kufia tumboni. Kutokana na hatari kubwa ya ugonjwa huu kwa wajawazito na watoto walio tumboni, ina...

Medical gamble that saved a little boy’s life

  The 18-month old boy was rushed to Muhimbili National Hospital (MNH) in Dar es Salaam where he was admitted. But his condition soon deteriorated into acute kidney failure. A dark cloud hovered over the family. The country’s biggest referral hospital has for years been infamous for being too ill-equipped to save those dying from such conditions. To read the whole story click here

Haya ndiyo madhara ya Kutumia earphones

Imeelezwa kuwa watu wanaotumia redio za simu wako hatarini kupatwa na ugonjwa wa saratani ya sikio na kichwa kutokana na mionzi mikali itokanayo na viselula hivyo. Akizungumza na FICHUO TZ, Dk. Leopard Mwinuka alisema, watakaoathirika na tatizo hilo ni wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikioni ‘headphone’. “Nawaonea huruma wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikio, kwani madhara yake hawawezi kuyaona sasa bali siku zijazo watapata ugonjwa wa saratani,” alisema Dk. Mwinuka. Alimaliza kwa kusema kuwa, mbali na kupata ugonjwa huo, wahusika wanaweza kupata tatizo la kutosikia vizuri kwa sababu, mtu anapotumia spika za sikio huweka sauti kubwa ili apate mdundo mzuri baada ya muda ngoma ya sikio inaathiriwa na hali hiyo. Habari nyingine za kitabibu zilisema kwamba, kwa kuwa pande zote za spika zina sumaku, huweza kuvutana na kuvuruga mpangilio wa ubongo hasa kama spika hizo zitakaa maskioni kwa zaidi ya sa...