Skip to main content

Vijue Vyakula Hatari kwa Kupunguza Nguvu za Kiume

Vijue Vyakula Hatari kwa Kupunguza Nguvu za Kiume
Mbegu za Flax (Flax seeds):  
Wanaume wanapaswa kufahamu aina ya vyakula ambavyo si rafiki kwao katika kuongeza kiwango cha homoni ya kiume iitwayo testosterone inayochochea sifa ya mwanaume yaani kuwa na nguvu za kiume. Baadhi ya vyakula visivyofaa kuliwa na mwanaume aliyetaka kuwa na nguvu za kiume ni vile vyenye asili ya homoni ya kike iitwayo estrogen. Hivyo sio kila vyakula vinafaa kwa mwanaume eti ilimradi tu vyakula hivyo vinasaidia kujenga mwili au kujaza tumbo wakati mtu akiwa na njaa.
Vyakula visivyofaa kabisa kuliwa na mwanaume kutokana na vyakula hivyo kupunguza homoni ya testosterone ni hivi vifuatavyo:
vyakula vinavyotengenezwa kutokana na unga wa mbegu za flax vimekuwa vikisifiwa kwa kuwa Omega-3 fats ambayo ni muhimu katika miili yetu. Hata hivyo mbegu za flax ni mbegu maarufu kwa kuwa na estrogen ambayo ni sawa kabisa na homoni ya estrogen iliyoko katika miili ya wanawake.
Flax seeds zina kiwango cha phytoestrogens mara tatu zaidi ya soya. Kama bado unafikiria kula vyakula vilivyo na mbegu za flax ili upate omega-3 achana na wazo hilo. Kama unataka kupata omega-3 kula samaki wenye mafuta mafuta (fish oils) utapata omega-3 ya kutosha.
Licorice: 
Huu ni mzizi ambao hutumika hasa kuondoa tatizo la msongo (stress) kwa watu wanaokumbwa na tatizo hilo. Pia mzizi huo hutumika kama sukari kwenye vinywaji kama chai au kahawa badala ya kutumia sukari ya kawaida.
Hata hivyo mzizi huu una estrogen ambayo hushusha kiwango cha homoni ya kiume ya testosterone kwa wanaume. Kuna utafiti ulifanywa ambapo wanaume 7 wenye afya walipewa gramu 7 za vidonge vya licorice kila mmoja kila siku.
Vidonge hivyo vilikuwa na kiasi cha gramu 0.5 za glycyrrhizic (kiambata kilichomo ndani ya licorice kinachopunguza testosterone kwa mwanaume). Baada ya siku 4 tu kiasi cha homoni ya testosterone kwa kila mwanaume aliyefanyiwa utafiti huo kilipungua kwa kiwango cha nusu ya kiasi cha homoni kwa kila mwanaume kilivyokuwa wakati wa kuanza utafiti.
Bia (Beer):
Sipendi kusema habari mbaya kwa wanywaji wa bia. Hata hivyo ni vema kusema ukweli kuhusu athari ya bia kwa wanaume. Bia imetengenezwa kwa humle (hops) ambayo kwa kiwango kikubwa inaleta hali ya homoni za kike kwa wanaume (highly estrogenic).
 Humle (Hops) ina kiasi cha 300,000 IU cha estrogen kwa kila gramu 100 za hops. Kabla ya mwaka 1487 bia ilikuwa ikitengenezwa kwa viambata (ingredients) ambazo zililenga kuifanya bia inaponywewa na mwanaume humfanya mwanaume awe na hali ya uanaume kweli kweli (more aggressive, horny, and socially dominant).
Hata hivyo baadaye Kanisa liliingilia uzalishaji wa bia na kutaka bia itengenezwe kwa viambata ambavyo vitamfanya mwanaume awe mpole au mtaratibu na sio mtu wa maguvu na ubabe ( to make men more feminine and sensitive). Hapo ndipo likazaliwa wazo la kutengeneza bia kwa kutumia humle (hops). Siku hizi bia hutengenezwa kwa viambata vitatu, hops, maji na malt.
Soya (Soy): 
Ina kiwango kikubwa cha Isoflavones ambayo ni kiuhalisia ni estrogen. Ulaji wa soya ni sawa na kula kidonge kimoja cha uzazi wa mpango (birth control pill). Kwa kuelewa zaidi madhara ya soya kwa wanaume soma hapa.
Spearmint:
Hutumiwa zaidi kama kiambata kwenye chewing gums, candies, na breath freshener au kwenye majani ya chai (herbal tea). Spearmint pia in akiwango kikubwa cha estrogen.
 Lima beans: 
Yana homoni za kike (estrogen) iitwayo inositol ambayo hupunguza kiwango cha homoni ya kiume (testosterone) kwa wanaume.
Whole grains:
 Ina gluten ambayo huongeza prolactin ambayo hupunguza kiasi cha testosterone.
 Soda: 
Unapenda kinywaji baridi yaani soda? Je unajua soda zimechangia sana tatizo la watu kuwa na unene au uzito uliopitiliza (obesity)? Tukiachana na suala la obesity hebu tuongelee kuhusu namna soda zinavyopunguza homoni za kiume (testosterone).
Chupa za plastiki ambazo hutumiwa na makampuni yanayotengeneza soda zimetengenezwa kwa phthalates ambayo hufanya plastiki ziweze kukunjwa katika umbo lolote (flexibility).
Phthalates ni estrogen! Kawaida ili kuondoa phthalates kwenye chupa za plastiki makampuni yanapaswa kuziacha chupa hizo zikae kwa mwaka mmoja bila kuweka soda ndani yake. Hata hivyo makampuni hayo mara tu baada ya kutengeneza chupa hizo huweka soda ndani yake na kuzipeleka sokoni kwa walaji.
Unajua nini kinatokea? Phthalates inaingia kwenye soda unayokunywa!!! Maana yake kama wewe ni mwanaume unaingiza homoni za kike mwilini mwako na matokeo yake unapunguza homoni za kiume!
Fast food: 
Wewe ni mwanaume unapenda kula chakula kwenye Mgahawa wa Fast Food? Ngoja nikupe maneno kwa nini usiwe na upungufu wa nguvu za kiume wakati unafakamia vyakula Fast Food. Ukienda Fast Food unaagiza vyakula vya nyama iwe ni beef au kuku au burger na unaagiza na soda then unaona mambo safi, sio? Haya hiyo nyama au kuku imetokana na wanyama waliofugwa na kulishwa junk grains na kupewa madawa kama antibiotics na homoni za kukuzia wanyama ambavyo vyote hivyo vina asili ya homoni za kike (estrogen).
Nyama hizo zinakaangwa au kupikwa kwa mafuta ya mimea kama vile soybean oil au sunflower oil ambayo yana estrogen! Baada ya hapo unashushia soda ambayo ina phthalates (homoni ya kike). Kwa ulaji huo unategemea kunako sita kwa sita uwe ‘super man’?!!

Comments

Popular posts from this blog

Kifafa cha Mimba (Preeclampsia, eclampsia)

MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes Kifafa cha mimba ni ugonjwa unaohusiana na msukumo mkubwa wa damu (high blood pressure) wakati wa ujauzito pamoja na kuharibika kwa viungo muhimu mwilini kama vile figo na ini. Kwa kawaida ugonjwa huu hutokea baada ya nusu ya kwanza ya ujauzito kuisha (kuanzia wiki ya 20 au miezi mitano ya ujauzito). Ugonjwa huu huweza kuwatokea hata wajawazito ambao hawakuwa na tatizo la msukumo mkubwa wa damu kabla ya ujauzito. Ugonjwa wa kifafa cha mimba unaweza kuleta madhara makubwa kwa mjamzito na mtoto aliye tumboni. Kuharibika kwa viungo muhimu kama figo na ini la mjamzito kunaweza kuwa kwa kiwango kikubwa kichoweza kusababisha mjamzito kupoteza maisha iwapo hatapata huduma ya afya mapema. Vilevile mtoto aliye tumboni anaweza kuathirika kwa kukosa damu ya kutosha toka kwa mama na kushindwa kukua vizuri na iwapo hali hiyo ikiendelea muda mrefu anaweza kufia tumboni. Kutokana na hatari kubwa ya ugonjwa huu kwa wajawazito na watoto walio tumboni, ina...

Medical gamble that saved a little boy’s life

  The 18-month old boy was rushed to Muhimbili National Hospital (MNH) in Dar es Salaam where he was admitted. But his condition soon deteriorated into acute kidney failure. A dark cloud hovered over the family. The country’s biggest referral hospital has for years been infamous for being too ill-equipped to save those dying from such conditions. To read the whole story click here

Haya ndiyo madhara ya Kutumia earphones

Imeelezwa kuwa watu wanaotumia redio za simu wako hatarini kupatwa na ugonjwa wa saratani ya sikio na kichwa kutokana na mionzi mikali itokanayo na viselula hivyo. Akizungumza na FICHUO TZ, Dk. Leopard Mwinuka alisema, watakaoathirika na tatizo hilo ni wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikioni ‘headphone’. “Nawaonea huruma wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikio, kwani madhara yake hawawezi kuyaona sasa bali siku zijazo watapata ugonjwa wa saratani,” alisema Dk. Mwinuka. Alimaliza kwa kusema kuwa, mbali na kupata ugonjwa huo, wahusika wanaweza kupata tatizo la kutosikia vizuri kwa sababu, mtu anapotumia spika za sikio huweka sauti kubwa ili apate mdundo mzuri baada ya muda ngoma ya sikio inaathiriwa na hali hiyo. Habari nyingine za kitabibu zilisema kwamba, kwa kuwa pande zote za spika zina sumaku, huweza kuvutana na kuvuruga mpangilio wa ubongo hasa kama spika hizo zitakaa maskioni kwa zaidi ya sa...