Skip to main content

USHAURI KWA WANAFUNZI WANAOTARAJIA KUOMBA VYUO VIKUU KUPITIA TCU 2016/2017

USHAURI KWA WANAFUNZI WANAOTARAJIA KUOMBA VYUO VIKUU KUPITIA TCU 2016/2017

Nachukua nafasi hii kuandika makala hii kuweza kutoa ushauri na kuweza kuwaeleza machache niyajuayo katika sakata zima la uombaji wa vyuo vikuu kupitia  TCU. Uombaji wa chuo ni swala nyeti ambalo linahitaji umakini na ushaur chanya kuweza kukamilisha mchakato huo kikamilifu.Yafuatayo ni mambo ambayo unapaswa kuzingatia katika uchaguzi wa chuo na fani tahasusi.

1) MATOKEO YAKO NDIO KIGEZO CHAKO: 

  Jambo la msingi kabisa ni kujitathmini kua kutokana na matokeo yangu haya naweza kusomea fani gani,na chuo gani ili kuweza kufikisha malengo yangu.Katika nukta hii napenda nigusie vitu vifuatavyo kwa ufupi kabisa.

         I.            Kwanza,nikupitia vizuri muongozo wa kitabu cha TCU,Hapo utapata kuoana orodha ya vyuo tafauti ,fani ,minimum entry requirements pamoja na gharama ya chuo husika.

       II.            Kutafuta washauri na wataalamu ambao wanaweza kukushauri vizuri kuhusu vyuo unavotaka kuomba fani na mengineyo ya msingi.

     III.            Usifuate mkumbo katika kuomba chuo :  hapa wengi huwaathiri huomba kwa kufuata rafiki yake kaomba vipi nayeye akafuata,ifahamike fika kua watu hutafautiana ki malengo,fikra lakini pia mnatafautiana pengine hata matokeo yenu,hivyo kwa hapa nitaendelea kusisitizia umuhim wa kupata washauri wazuri .

 

2) UPANGAJI WA FANI NA CHUO HUSIKA KULINGANA NA PRIORITY

Hii  ni moja kati ya nukta muhimu sana ambayo inahitaji umakini mkubwa katika mchakato mzima wa uombaji wa chuo.

Mwanafunzi hupewa nafasi tano za kufanya udahili kutokana na fani azitakazo ,ambazo hapa unatakiwa uzipange fani hizo katika mpangilio wa priority yako.Mambo ya kuzingatia :-

         I.            Hakikisha ile fani ya mwanzo kabisa uipendayo katika chuo utakacho unaiweka hapa,

Mara nyingi ikiwa matokeo yako yanaruhusu katika chuo hicho kwa kuzingatia competition ilokuwepo na idadi ya wanafunzi watanaotakiwa basi  inakua asilimia kubwa kukipata.

Ø  Hakikisha hapa usiweke chuo ambacho kwa matokeo yako na vigezo vitakiwavyo una uhakika wa kukosa,kua makini sana katika sehemu hii.

       II.            Baada ya kuchagua fani ya kwanza,basi utachagua fani na chuo katika sehemu nne zilizobaki kwa kuzingatia priority yako,vigezo vya chuo na matokeo yako.

     III.            Nashauri ,kutokana na matokeo yako husika jaribu sana kuangalia competition ya chuo,idadi ya wanafunzi wanavohitajika na vigezo ,jaribu kuepuka kuomba chuo ambacho una uhakika hupati mfano mzuri ,kuna wimbi la wanafunzi wa PCB ambao hutaka kusomea udaktar i(medicine)  katika chuo cha MUHIMBILI,hapo uwe makini sana kwani chuo hicho kwa udaktari wanachkua division one tena iliyochangamka….

    IV.            Selection mara nyingi wanaangalia kigezo cha,cut off point, matokeo na  priority hivyo usishangae wewe na mwenzako matokeo sawa mkaomba kozi sawa lkn mpangilio tafauti lakin mmoja akapata kuchaguliwa mmoja akakosa kuchaguliwa katika raund ya kwanza,katika hili naendelea kusisitiza kuhusu ushauri kwa wenye uzoefu wa kufanya application hizo.

Angalizo: kua na minimum entry requirements katika chuo husika c sababu ya lazima kupata chuo .

Kuna factors nyingi ambazo zinachangia kama competition ya waombaji,idadi ya wanafunzi wanaohitajika katika kila fani, priority arrangements etc.

3. KUA TAYARI KUSOMA  KATIKA FANI NA CHUO CHOCHOTE AMBACHO UTAKIOMBA

Kabla ya kuomba nafasi hizo tano basi ujikubalishe kua katika nafasi hizo  popote utakapochaguliwa utasoma.Katika nukta hii  natilia umuhim wa kua tayari kusoma popote utakapopangiwa kwani mchakato wa kudahili ni mrefu sana ambao unazingatia vigezo tafauti,hivyo unaweza kuchaguliwa nafasi hata ya tano uliyoomba,hivyo kwa kuepusha usumbufu wa baadae hakikisha unajitathimini vizuri kwanza katika selection  yako.

 

4) KUCHAGUA CHUO AMBACHO UNAWEZA KUKILIPIA GHARAMA ZAKE ZA ADA BAADA YA KUPATA ASILIMIA YA MKOPO KUTOKA BODI YA MKOPO

Vyuo vipo vya serekali na private ,mara nyingi vyuo vya serekali ada ya chuo ni ndogo kulinganisha na private.

Hivyo nashauri,kwanza uangalie chuo unachotaka kukiomba ada yake,na asilimia ya mkopo ambao bodi wanakupatia,hivyo utapata kujitathmini na familia yako kua unaweza kulipia asilimia iliobaki au laa.

Hapa napo panahitaji umakini mkubwa ,kwani kuna wimbi la wanafunzi kila mwaka wanapata chuo lakini wanagundua ada ya chuo kikubwa sana ambacho hawawezi kukimudu hivyo wanaamua kuhairisha mwaka kuomba tena vyuo vyengine kwa mwaka mwengine.

 

5) Kuzingatia soko la ajira

Kama tujuavyo tunasoma lakini malengo yetu at the end of the day ni kupata ajira na si kumaliza na mavyeti na kubaki nayo nyumbani.Binafsi mimi si mtaalamu sana katika sehemu hii hivyo ninachoweza kukwambia nakuachia nukta hii uitafute kwa washauri wako na kwa watu wako wakaribu.

Kwa kweli yapo mengi sana ya kuzingatia lakin  mengine utapatiwa na washauri wako ,lakini ningependa nigeuze upande wa pili wa shilingi ni nizungumzie kwa ufupi sana mambo ambayo yanaweza kujitokeza ukikosa umakini katika mchakato huu.

        I.            Kukosa nafasi zote tano ulizoziomba.

Matokeo yanaweza kutoka na kujikuta umekosa nafasi zote ulizoomba na  hivo kutakiwa kufanya tena application katika raund nyengne,mwaka jana wanafunzi walifanya selection  mpaka raund sita.

 

      II.            Kupata fani mbovu ambayo hukuitegemea kabisa.

   III.            Kughairisha mwaka baada ya kutoridhishwa na mchakato wa chuo ulichopata au fani uliopangiwa

    IV.            Kukosa chuo moja kwa moja.

Naomba nisikuchoshe kwa kukujazia mambo mingi sana katika Makala hii ,naomba uzingatie vizuri maelezo niliyoyatoa  huo ni ushauri wangu tu kutokana na experience niliyoipata. Nimeandika Makala hii kwa kuona ipo haja ya kuwashauri wenzangu kua na tahadhari kwani waswahili husema “KINGA NI BORA KULIKO TIBA’’

       Brought to you By DR FOC
PREP BY MASATU.


Comments

Popular posts from this blog

Kifafa cha Mimba (Preeclampsia, eclampsia)

MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes Kifafa cha mimba ni ugonjwa unaohusiana na msukumo mkubwa wa damu (high blood pressure) wakati wa ujauzito pamoja na kuharibika kwa viungo muhimu mwilini kama vile figo na ini. Kwa kawaida ugonjwa huu hutokea baada ya nusu ya kwanza ya ujauzito kuisha (kuanzia wiki ya 20 au miezi mitano ya ujauzito). Ugonjwa huu huweza kuwatokea hata wajawazito ambao hawakuwa na tatizo la msukumo mkubwa wa damu kabla ya ujauzito. Ugonjwa wa kifafa cha mimba unaweza kuleta madhara makubwa kwa mjamzito na mtoto aliye tumboni. Kuharibika kwa viungo muhimu kama figo na ini la mjamzito kunaweza kuwa kwa kiwango kikubwa kichoweza kusababisha mjamzito kupoteza maisha iwapo hatapata huduma ya afya mapema. Vilevile mtoto aliye tumboni anaweza kuathirika kwa kukosa damu ya kutosha toka kwa mama na kushindwa kukua vizuri na iwapo hali hiyo ikiendelea muda mrefu anaweza kufia tumboni. Kutokana na hatari kubwa ya ugonjwa huu kwa wajawazito na watoto walio tumboni, ina...

Medical gamble that saved a little boy’s life

  The 18-month old boy was rushed to Muhimbili National Hospital (MNH) in Dar es Salaam where he was admitted. But his condition soon deteriorated into acute kidney failure. A dark cloud hovered over the family. The country’s biggest referral hospital has for years been infamous for being too ill-equipped to save those dying from such conditions. To read the whole story click here

Haya ndiyo madhara ya Kutumia earphones

Imeelezwa kuwa watu wanaotumia redio za simu wako hatarini kupatwa na ugonjwa wa saratani ya sikio na kichwa kutokana na mionzi mikali itokanayo na viselula hivyo. Akizungumza na FICHUO TZ, Dk. Leopard Mwinuka alisema, watakaoathirika na tatizo hilo ni wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikioni ‘headphone’. “Nawaonea huruma wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikio, kwani madhara yake hawawezi kuyaona sasa bali siku zijazo watapata ugonjwa wa saratani,” alisema Dk. Mwinuka. Alimaliza kwa kusema kuwa, mbali na kupata ugonjwa huo, wahusika wanaweza kupata tatizo la kutosikia vizuri kwa sababu, mtu anapotumia spika za sikio huweka sauti kubwa ili apate mdundo mzuri baada ya muda ngoma ya sikio inaathiriwa na hali hiyo. Habari nyingine za kitabibu zilisema kwamba, kwa kuwa pande zote za spika zina sumaku, huweza kuvutana na kuvuruga mpangilio wa ubongo hasa kama spika hizo zitakaa maskioni kwa zaidi ya sa...