Skip to main content

WANANCHI WA KIJIJI CHA ILININDA WILAYANI LUDEWA WACHANGISHANA PESA MIFUKONI MWAO ILI KUKARABATI BARABARA

MTU KWAO/ Eagle Eyes

WANANCHI WA KIJIJI CHA ILININDA WILAYANI LUDEWA WACHANGISHANA PESA MIFUKONI MWAO ILI KUKARABATI BARABARA,

Na Maiko Luoga Ludewa,
Barabara ya Kutoka Kijiji cha ilawa Hadi Ilininda wilayani Ludewa imedumu kwa Muda mrefu ikiwa mbovu bila matengenezo Hatimaye Wananchi Wa Kijiji cha Ilininda kwakushirikiana na Wadau mbalimbali ndani ya Kata ya Madilu Wilayani Ludewa katika Mkoa Wa Njombe wameamua Kuingia Mifukoni mwao na Kuchangishana Pesa kwa Umoja wao ili kuikarabati barabara hiyo Bila kuisubiri Serikali.
Wakizungumza na Mwandishi wetu wananchi Wa Kijiji cha Ilininda wamesema Baada ya Kuona barabara yao Ipo katika hali mbaya wameweza kushirikiana na Uongozi Wa NGO ya IDEFO hadi kuchangia kiasi cha Sh. 15 million Ambazo tayari zimetumika Kulipia mafuta Kwa mtu aliyewasaidia kupata Mashine na Uchimbaji Wa Barabara hiyo unaendelea Huku wakiiomba Serikali kuwasaidia Pesa kwaajili ya Kuendelea Kuikarabati barabara hiyo waliyoamua kuichimba kwa Nguvu zao wenyewe.
Mh. John Mkolwe ni Diwani Wa Kata ya Madilu Amesema kuwa Mbunge Wa jimbo la Ludewa Mh. Deo Ngalawa amewaunga mkono wananchi kwakutoa kias cha sh. Lakitano Huku akieleza mgawanyo Wa Mchango kwa wananchi kwakusema wananchi Wa kipato cha kawaida wanachangia kias cha Sh. 20,000 na kuendelea na wale wenye kipato cha juu zaidi wanachangia kias cha Sh. Lakimoja na kuendelea Pia amesema wamemuandikia Barua mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Ludewa Ili kuomba msaada zaidi lakini barua hiyo bado haijajibiwa.
Kutoka katika kijiji cha Ilawa hadi Ilininda wilayani Ludewa kunajumla ya Klomita 14 ambapo kwakutumia Pesa hiyo Wamefanikisha kuchimba jumla ya Klomita 10 na kazi inaendelea Huku Kaimu Katibu Wa (IDEFO) bw. Deograsias Mgina Akisema kuwa Bado wanakabiliwa na Changamoto ya PESA zaidi kwaajili ya Kuweka kifusi na kushindilia Barabara hiyo ili iweze kupitika angalau kwa Mda mrefu zaidi.
Uongozi huo Wa Kata ya Madilu kwakushirikiana na wananchi pamoja na wadau mbalimbali wanawaomba Wafadhiri, Taasisi mbalimbali na wadau tofauti kuwasaidia Ili kuweza kukamilisha Ukarabati Wa barabara hiyo ambayo inafaida kubwa kwa wananchi Ambao ni wakulima na wafugaji Wenye kipato cha chini zaidi kiuchumi kwakuwa kwakufanya hivyo nikuwainua wanainchi hao

Comments

Popular posts from this blog

Kifafa cha Mimba (Preeclampsia, eclampsia)

MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes Kifafa cha mimba ni ugonjwa unaohusiana na msukumo mkubwa wa damu (high blood pressure) wakati wa ujauzito pamoja na kuharibika kwa viungo muhimu mwilini kama vile figo na ini. Kwa kawaida ugonjwa huu hutokea baada ya nusu ya kwanza ya ujauzito kuisha (kuanzia wiki ya 20 au miezi mitano ya ujauzito). Ugonjwa huu huweza kuwatokea hata wajawazito ambao hawakuwa na tatizo la msukumo mkubwa wa damu kabla ya ujauzito. Ugonjwa wa kifafa cha mimba unaweza kuleta madhara makubwa kwa mjamzito na mtoto aliye tumboni. Kuharibika kwa viungo muhimu kama figo na ini la mjamzito kunaweza kuwa kwa kiwango kikubwa kichoweza kusababisha mjamzito kupoteza maisha iwapo hatapata huduma ya afya mapema. Vilevile mtoto aliye tumboni anaweza kuathirika kwa kukosa damu ya kutosha toka kwa mama na kushindwa kukua vizuri na iwapo hali hiyo ikiendelea muda mrefu anaweza kufia tumboni. Kutokana na hatari kubwa ya ugonjwa huu kwa wajawazito na watoto walio tumboni, ina...

Medical gamble that saved a little boy’s life

  The 18-month old boy was rushed to Muhimbili National Hospital (MNH) in Dar es Salaam where he was admitted. But his condition soon deteriorated into acute kidney failure. A dark cloud hovered over the family. The country’s biggest referral hospital has for years been infamous for being too ill-equipped to save those dying from such conditions. To read the whole story click here

Haya ndiyo madhara ya Kutumia earphones

Imeelezwa kuwa watu wanaotumia redio za simu wako hatarini kupatwa na ugonjwa wa saratani ya sikio na kichwa kutokana na mionzi mikali itokanayo na viselula hivyo. Akizungumza na FICHUO TZ, Dk. Leopard Mwinuka alisema, watakaoathirika na tatizo hilo ni wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikioni ‘headphone’. “Nawaonea huruma wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikio, kwani madhara yake hawawezi kuyaona sasa bali siku zijazo watapata ugonjwa wa saratani,” alisema Dk. Mwinuka. Alimaliza kwa kusema kuwa, mbali na kupata ugonjwa huo, wahusika wanaweza kupata tatizo la kutosikia vizuri kwa sababu, mtu anapotumia spika za sikio huweka sauti kubwa ili apate mdundo mzuri baada ya muda ngoma ya sikio inaathiriwa na hali hiyo. Habari nyingine za kitabibu zilisema kwamba, kwa kuwa pande zote za spika zina sumaku, huweza kuvutana na kuvuruga mpangilio wa ubongo hasa kama spika hizo zitakaa maskioni kwa zaidi ya sa...