Skip to main content

Polisi wakamata vipande vya meno ya Tembo 666 vyenye thamani ya zaidi ya sh. bilioni nne 1week ago

Polisi wakamata vipande vya meno ya Tembo 666 vyenye thamani ya zaidi ya sh. bilioni nne
1week ago

  Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Kamishna Diwani Athuman akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijiji Dar es Salaam leo, kuhusu Jeshi la Polisi kutokubali kuona kundi la watu wachache linatishia usalama wa maisha ya raia na mali zao, Wote watakaobainika kuwa ni wahalifu watakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Waandishi wa habari wakimsikiliza Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Kamishna Diwani Athuman leo jijini Dar es Salaam.
(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii)

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
JESHI la Polisi  nchini kwa kishirikiana na Ofisi za Interpol Kanda ya Kusini Mwa Afrika imefanya operesheni  na kukamata vipande vya meno ya Tembo 666 vyenye uzito wa Kilogram 1279.19 vyenye thamani zaidi ya a Sh. Biloni Nne.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Kamishna wa  Jeshi  la Polisi (CP), Diwani Athuman wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, amesema kuwa vipande hivyo vya tembo yamehusisha watu tisa  kati yao mmoja ni Raia wa Guinea na mwingine ni Raia wa Uganda.

Amesema kuwa katika operesheni Usalama  III wameweza kukamata  vitu mbalimbali kutokana na taarifa za kiitelijensia zilizokusanywa wakati wa matayarisho ya operesheni ya Usalama III, ambapo waliweza kukamata mitambo ya 18 ya kutengenezea gongo pamoja na  lita  za gongo  960  zimekamatwa.

Athuman amesema katika Operesheni  hiyo wameweza kukamata watuhumiwa 265  ambapo baada ya uchunguzi wataobainika  kuhusika na  vitendo vya kihalifu watafikishwa mahakamani mara moja ikiwa namna au nyingine katika kufankisha vitendo vya kihalifu.

Kamishina Othman amesema ametoa rai kwa wanunuzi wa magari nje ya nchi kuwasiliana na ofisi za Interpol za ndani au nje ya nchi magari yanakotoka kwa uchunguzi kabla ya kuyanunua ili kuondoa usumbufu wa kukamatwa mara kwa mara katika operesheni  kama hizi.

Amesema kutokana na operesheni hiyo jeshi la polisi halitakubali kuona kundi la watu wachache linalotishia usalama maisha raia wema na  mali zao na wataobainika kufanya hivyo kuchukuliwa hatua za kisheria bila kusita.

Comments

Popular posts from this blog

Kifafa cha Mimba (Preeclampsia, eclampsia)

MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes Kifafa cha mimba ni ugonjwa unaohusiana na msukumo mkubwa wa damu (high blood pressure) wakati wa ujauzito pamoja na kuharibika kwa viungo muhimu mwilini kama vile figo na ini. Kwa kawaida ugonjwa huu hutokea baada ya nusu ya kwanza ya ujauzito kuisha (kuanzia wiki ya 20 au miezi mitano ya ujauzito). Ugonjwa huu huweza kuwatokea hata wajawazito ambao hawakuwa na tatizo la msukumo mkubwa wa damu kabla ya ujauzito. Ugonjwa wa kifafa cha mimba unaweza kuleta madhara makubwa kwa mjamzito na mtoto aliye tumboni. Kuharibika kwa viungo muhimu kama figo na ini la mjamzito kunaweza kuwa kwa kiwango kikubwa kichoweza kusababisha mjamzito kupoteza maisha iwapo hatapata huduma ya afya mapema. Vilevile mtoto aliye tumboni anaweza kuathirika kwa kukosa damu ya kutosha toka kwa mama na kushindwa kukua vizuri na iwapo hali hiyo ikiendelea muda mrefu anaweza kufia tumboni. Kutokana na hatari kubwa ya ugonjwa huu kwa wajawazito na watoto walio tumboni, ina...

Medical gamble that saved a little boy’s life

  The 18-month old boy was rushed to Muhimbili National Hospital (MNH) in Dar es Salaam where he was admitted. But his condition soon deteriorated into acute kidney failure. A dark cloud hovered over the family. The country’s biggest referral hospital has for years been infamous for being too ill-equipped to save those dying from such conditions. To read the whole story click here

Haya ndiyo madhara ya Kutumia earphones

Imeelezwa kuwa watu wanaotumia redio za simu wako hatarini kupatwa na ugonjwa wa saratani ya sikio na kichwa kutokana na mionzi mikali itokanayo na viselula hivyo. Akizungumza na FICHUO TZ, Dk. Leopard Mwinuka alisema, watakaoathirika na tatizo hilo ni wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikioni ‘headphone’. “Nawaonea huruma wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikio, kwani madhara yake hawawezi kuyaona sasa bali siku zijazo watapata ugonjwa wa saratani,” alisema Dk. Mwinuka. Alimaliza kwa kusema kuwa, mbali na kupata ugonjwa huo, wahusika wanaweza kupata tatizo la kutosikia vizuri kwa sababu, mtu anapotumia spika za sikio huweka sauti kubwa ili apate mdundo mzuri baada ya muda ngoma ya sikio inaathiriwa na hali hiyo. Habari nyingine za kitabibu zilisema kwamba, kwa kuwa pande zote za spika zina sumaku, huweza kuvutana na kuvuruga mpangilio wa ubongo hasa kama spika hizo zitakaa maskioni kwa zaidi ya sa...