Skip to main content

AINA ZA UPUNGUFU WA DAMU MWILINI (ANAEMIA)


MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes
Leo tuangalie tatizo la upungufu wa damu mwilini. Anaemia ni jina la jumla linalotumiwa kubainisha aina mbalimbali za upungufu wa damu mwilini.
Kiwango cha kawaida cha chembe nyekundu za damu (Haemoglobin-Hb) katika mwili wa binadamu ni kati ya gramu 12 mpaka 14 kwa kila mililita ya damu na zikiwa pungufu ya hapo mtu huyo anakuwa na tatizo la upungufu wa damu.
Upungufu wa damu mwilini hutokea iwapo mkusanyiko wa pamoja wa chembe nyekundu za damu zinapopungua kupita kiwango cha kawaida kinachotakiwa kwenye mwili wa binadamu.
Tatizo hili linaweza kumpata mtu yeyote ingawa visababishi vinaweza kutofautiana.
Licha ya utofauti huo mara nyingi tatizo hili husababishwa na mambo makuu matatu ambayo ni kupoteza damu mfano wakati wa hedhi kwa wanawake hasa wanaotokwa na damu nyingi au kuvuja damu kunakosababishwa na vidonda vya tumbo.
Sababu nyingine ni uzalishwaji duni wa chembe nyekundu za damu unaosababishwa na upungufu wa vitamini au lishe duni pamoja na magonjwa sugu. Pia magonjwa ya kurithi.
Iwapo mtu atapungukiwa kiasi cha madini, ulaji wa madini ya chuma katika mlo wa kawaida wa mtu hauwezi kufidia kiwango cha madini kilichopotea na kiasi hicho kinachokuwa kimebaki hutumika mara moja.
Aina za upungufu wa damu mwilini
Zipo aina mbalimbali za upungufu wa damu ikiwemo Haemolytic Anaemia. Hali hii ya upungufu wa damu, chembe nyekundu za damu huharibiwa haraka kuliko mwili unavyoweza kuzalisha chembe nyingine.
Upungufu huu husababishwa na mambo mengi ikiwemo kansa aina ya Lymphoma au utumiaji wa baadhi ya dawa ambazo huweza kuangamiza chembe nyekundu za damu kwa mfano dawa aina ya Methylodopa inayotibu matatizo ya presha ya kupanda.
Mtu mwenye aina hii ya upungufu wa damu anaweza kupatwa na homa, kutetemeka kwa mwili, maumivu ya tumbo na mgongo na mapigo ya moyo kushuka ghafla.
Pernicious Anaemia. Huu ni upungufu wa damu unaotokana na ukosefu wa kutosha wa asidi aina ya Folic (Folate) katika chakula.
Asidi aina ya Folate hupatikana katika mbogamboga za rangi ya kijani, matunda na nyama.Aplastica Anaemia. Huu ni upungufu wa damu unaotokea wakati chembe nyekundu za damu zinaposhindwa kuzalishwa ipasavyo.
Sickle cell Anaemia.
Ni aina nyingine ya upungufu wa damu ambao chembe nyekundu za damu huwa na muundo usio wa kawaida unaozuia na kuathiri mishipa midogo ya damu na hivyo kusababisha kuziba kwa mishipa hiyo ya damu.
Dalili za upungufu wa damu mwilini (anaemia)
Mtu mwenye tatizo la upungufu wa damu mara nyingi huwa amepauka mwili na hujisikia kuchoka, udhaifu na huwa na mwendo kasi wa damu (yaani high pulse rate). Mgonjwa kuhisi kiu, kizunguzungu wakati akisimama, moyo kwenda kasi wakati akitumia nguvu kufanya jambo lolote, kuhema mfululizo na kupumua haraka haraka.
Dalili nyingine ni mapigo ya moyo kwenda kwa kasi, kuhisi uchovu sana au hata kuishiwa kabisa na nguvu. Wakati mwingine mgonjwa anaweza kuhisi maumivu ya kifua pamoja na kuchanganyikiwa anaposhughulikia jambo fulani.
Kuvimba kwa tumbo au sehemu za chini yake, kupoteza nguvu na macho kukosa nuru ya kuona vizuri ni dalili nyingine za mtu mwenye tatizo hili.
Matibabu yake
Matibabu ya upungufu wa damu aina yoyote yanategemea aina ya upungufu wa damu inayomkabili mgonjwa.
Upungufu wa damu hutibiwa mapema kwa kubadili lishe pamoja na kuongeza lishe yenye vitamini C na B12 pamoja na madini ya chuma kutokana na visababishi vya tatizo.
Matibabu ya lishe yanaweza kutumika kwa ushauri wa daktari ingawa yanaweza yasitoshe hadi pale mgonjwa atakapoongezewa damu.
Mara nyingine vidonge na sindano zenye lishe hizo huweza kutumiwa na madaktari hospitalini sambamba na matibabu ya tatizo linalosababisha na iwapo mgonjwa yuko mahututi huweza kuongezewa damu. Ushauri, ukiona dalili hizo, muone daktari haraka
AINA ZA UPUNGUFU WA DAMU MWILINI 
Katika makala ya wiki iliyopita tuliangazia tatizo la upungufu wa damu mwilini wengine huita Anaemia ambalo ni jina la jumla linalotumiwa kubainisha aina mbalimbali za upungufu wa damu mwilini.
Tukasema kiwango cha kawaida cha chembe nyekundu za damu (Hb) katika mwili wa binadamu ni kati ya gramu 12 mpaka 14 kwa kila milimita ya damu, zikiwa pungufu ya hapo mtu huyo anakuwa na tatizo la upungufu wa damu.
Tulitaja aina za upungufu wa damu kama vile Pernicious Anaemia na Aplastica Anaemia. Sasa endelea…
Sickle Cell Anaemia:
Ni aina nyingine ya upungufu wa damu ambao chembe nyekundu za damu huwa na muundo usio wa kawaida unaozuia na kuathiri mishipa midogo ya damu na hivyo kusababisha kuziba kwa mishipa hiyo ya damu.
DALILI ZA UPUNGUFU WA DAMU
Mtu mwenye tatizo la upungufu wa damu mara nyingi huwa amepauka mwili na viganja na kucha kuwa nyeupe na hujisikia kuchoka, udhaifu na huwa na mwendo kasi wa damu (yaani High Pulse Rate) na macho yake huwa meupe.
Dalili nyingine ni mgonjwa kuhisi kiu, kizunguzungu wakati akisimama, kuwa na mahangaiko ya moyo wakati akitumia nguvu kufanya jambo lolote, kuhema mfululizo na kupumua harakaharaka, mapigo ya moyo kwenda kwa kasi, kuhisi uchovu au hata kuishiwa kabisa na nguvu.
Dalili nyingine ni kusikia maumivu ya kifua pamoja na akili yake kushindwa kufikiri sawasawa, vilevile kuvimba kwa tumbo au sehemu za chini yake, kupoteza nguvu na macho kukosa nuru ya kuona vizuri.
VIPIMO NA MATIBABU
Uchunguzi wa wingi wa damu hufanyika kwa kupima kiasi cha mkusanyiko wa pamoja wa chembe nyekundu za damu kitaalamu huitwa Haemoglobin pamoja na kufanya kipimo kingine cha damu kijulikanacho kama Peripheral Smear.
Vipimo vingine vya maabara ni pamoja na kipimo cha kufahamu uwezo wa kuhifadhi madini ya chuma yaani Total Iron Binding Capacity (TIBC), kiasi cha Feritin katika damu pamoja na kiasi cha
Folic Acid.
Aidha, katika mazingira mengine kipimo cha kuchukua sehemu ya supu ya mifupa na kuichunguza maabara yaani (Bone Marrow Biopsy) kinaweza kufanywa, japo si mara kwa mara.
Matibabu ya upungufu wa damu aina yoyote yanategemea aina ya upungufu wa damu unaomkabili mgonjwa.
Upungufu wa damu hutibiwa mapema kwa kubadili lishe pamoja na kuongeza lishe yenye vitamini C na B12 pamoja na madini ya chuma kutokana na visababishi vya tatizo.
Licha ya hiyo, matibabu ya lishe yanaweza kutumika kwa ushauri wa daktari ingawa yanaweza yasitoshe hadi pale mgonjwa atakapoongezewa damu.
Mara nyingine vidonge na sindano zenye lishe hizo huweza kutumiwa na madaktari hospitalini sambamba na matibabu ya tatizo linalosababisha, iwapo mgonjwa yuko katika hali ya mahututi huweza kuongezewa damu.
Tatizo la upungufu wa damu ni tatizo la hatari sana endapo mwenye tatizo hilo atachelewa kupata matibabu mapema. Ukiona dalili hizo wahi kumuona daktari.

Comments

Popular posts from this blog

Kifafa cha Mimba (Preeclampsia, eclampsia)

MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes Kifafa cha mimba ni ugonjwa unaohusiana na msukumo mkubwa wa damu (high blood pressure) wakati wa ujauzito pamoja na kuharibika kwa viungo muhimu mwilini kama vile figo na ini. Kwa kawaida ugonjwa huu hutokea baada ya nusu ya kwanza ya ujauzito kuisha (kuanzia wiki ya 20 au miezi mitano ya ujauzito). Ugonjwa huu huweza kuwatokea hata wajawazito ambao hawakuwa na tatizo la msukumo mkubwa wa damu kabla ya ujauzito. Ugonjwa wa kifafa cha mimba unaweza kuleta madhara makubwa kwa mjamzito na mtoto aliye tumboni. Kuharibika kwa viungo muhimu kama figo na ini la mjamzito kunaweza kuwa kwa kiwango kikubwa kichoweza kusababisha mjamzito kupoteza maisha iwapo hatapata huduma ya afya mapema. Vilevile mtoto aliye tumboni anaweza kuathirika kwa kukosa damu ya kutosha toka kwa mama na kushindwa kukua vizuri na iwapo hali hiyo ikiendelea muda mrefu anaweza kufia tumboni. Kutokana na hatari kubwa ya ugonjwa huu kwa wajawazito na watoto walio tumboni, ina...

Medical gamble that saved a little boy’s life

  The 18-month old boy was rushed to Muhimbili National Hospital (MNH) in Dar es Salaam where he was admitted. But his condition soon deteriorated into acute kidney failure. A dark cloud hovered over the family. The country’s biggest referral hospital has for years been infamous for being too ill-equipped to save those dying from such conditions. To read the whole story click here

Haya ndiyo madhara ya Kutumia earphones

Imeelezwa kuwa watu wanaotumia redio za simu wako hatarini kupatwa na ugonjwa wa saratani ya sikio na kichwa kutokana na mionzi mikali itokanayo na viselula hivyo. Akizungumza na FICHUO TZ, Dk. Leopard Mwinuka alisema, watakaoathirika na tatizo hilo ni wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikioni ‘headphone’. “Nawaonea huruma wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikio, kwani madhara yake hawawezi kuyaona sasa bali siku zijazo watapata ugonjwa wa saratani,” alisema Dk. Mwinuka. Alimaliza kwa kusema kuwa, mbali na kupata ugonjwa huo, wahusika wanaweza kupata tatizo la kutosikia vizuri kwa sababu, mtu anapotumia spika za sikio huweka sauti kubwa ili apate mdundo mzuri baada ya muda ngoma ya sikio inaathiriwa na hali hiyo. Habari nyingine za kitabibu zilisema kwamba, kwa kuwa pande zote za spika zina sumaku, huweza kuvutana na kuvuruga mpangilio wa ubongo hasa kama spika hizo zitakaa maskioni kwa zaidi ya sa...