Skip to main content

Wanafunzi Vyuo Vikuu ‘wanakula nyasi?’



Wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es salaam wakiwa katika mgomo
Wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es salaam wakiwa katika mgomo


Kitendo hiki ni kinyume na mkataba baina ya wanafunzi hao na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya juu hapa nchini (HESLB) lakini pia ni kinyume na ahadi ya serikali iliyotolewa wiki mbili zilizopita kuwa wanafunzi hao wangepewa fedha za kujikimu kwaajili ya mafunzo kwa vitendo kabla ya 8 Agosti mwaka huu.
Katika mkutano na vyombo vya habari, wiki mbili zilizopita Prof. Joyce Ndalichako Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia alidai kuwa serikali imeshindwa kuwapa wanafunzi fedha za mafunzo kwa vitendo kutokana na zoezi la kuhakiki wanafunzi hewa na kwamba imesogeza mbele kuanza kwa zoezi hilo la kitaaluma kutoka 25 Julai mwaka huu mpaka 08 Agosti mwaka huu.
Prof. Ndalichako aliahidi kuwa wanafunzi wa Vyuo Vikuu kote nchini ambao ni wanufaika wa mikopo wangepewa fedha hizo kabla ya Agosti 08 mwaka huu, jambo ambalo limeshindikana mpaka sasa huku waziri huyo akishindwa kutoa ufafanuzi juu ya wanafunzi kuanza mafunzo kwa vitendo bila fedha za kujikimu jambo linalowapa wakati mgumu.
Tangazo lililotolewa 4 Agosti mwaka huu na utawala wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kupitia kwa Profesa Florens Luoga ambaye ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo anayeshughulikia masuala ya taaluma limewataka wanafunzi wote wa Chuo hicho kuripoti katika vituo vyao vya mafunzo kwa vitendo huku likidokeza kuwa serikali itawalipa fedha zao za kujikimu kwa awamu (installments).
Agizo hilo limewafanya wanafunzi hao kuanza mafunzo kwa vitendo huku Serikali yao ya Wanafunzi (DARUSO) ikitoa matamko mawili ya kujikanganya ambapo katika tamko lililotolewa kwa wanahabari na Erasmi Leon 06 Agosti mwaka huu aliwasihi wanafunzi hao kugomea kuanza mafunzo kwa vitendo bila kupata fedha zao lakini siku moja baadaye alitoa tangazo lingine akiwataka wanafunzi hao kuanza zoezi la mafunzo kwa vitendo bila kubainisha ni lini watapokea fedha zao.
Prof. Ndalichako amenukuliwa hivi karibuni akisema Serikali tayari imeshaidhinisha malipo hayo na kwamba mchakato wa malipo katika akaunti za wanafunzi upo mikononi mwa bodi ya mikopo, hata hivyo Mwanahalisi online ilipomtafuta Kaimu Mkurugenzi wa HESLB hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo na kuomba mwandishi amtafute ofisa mawasiliano wa HESLB Cosmas Mwaisobwa ambaye hata hivyo hakuweza kupatikana.
Hata hivyo taarifa zilizotolewa na mmoja wa maofisa wa bodi ya mikopo ambaye hakutaka kutajwa kwa madai kuwa yeye si msemaji zinasema kuwa serikali ipo hoi kifedha ndiyo maana imechelewesha kutoa fedha kwa bodi hiyo ili ziweze kuwafikia wanafunzi.
“Ndugu yangu sisi HESLB tunasingiziwa tu, serikali haina fedha uhakiki wa wanafunzi hewa umeshamalizika muda mrefu lakini wakatuambia hawana fedha za kuwapa wanafunzi na inabidi walipwe nusu nusu tofauti na utaratibu wa miaka mingine ambayo tulikuwa tunawalipa fedha zote, sasa hivi ndiyo tupo kwenye mchakato wa kuvipelekea vyuo vyote fedha hizo,” amedokeza.
Hii siyo mara ya kwanza kwa serikali kuwalazimisha wanafunzi kwenda katika mafunzo kwa vitendo bila kuwapa fedha zao za kujikimu kama mikataba yao na bodi ya mikopo inavyoelekeza.
Mwaka 2014 wanafunzi hao waliwahi kucheleweshewa malipo hayo kwa zaidi ya mwezi mmoja huku serikali ikidai kutokuwa na fedha hata hivyo hali hii haikutarajiwa kujitokeza katika wakati huu kutokana na serikali kujinadi mara kwa mara kuwa imepandisha ukusanyaji wa mapato kutoka wastani wa 800 bilioni kwa mwezi mpaka kufikia zaidi ya 1.2 trilioni.
Itakumbukwa kuwa kutochelewesha mikopo kwa wanafunzi wa Vyuo Vikuu ilikuwa ni miongoni mwa ahadi za mara kwa mara za Rais John Magufuli wakati akiwania nafasi ya urais mwishoni mwa mwaka jana na zaidi ya yote alijiapiza kuwa angemfukuza kazini mtumishi yoyote wa umma ambaye angesababisha kucheleweshwa kwa fedha hizo za wanafunzi wa vyuo vikuu.
Hata hivyo hali imekuwa tofauti. Hakuna mtumishi wa serikali aliyefukuzwa. Kilichoahidiwa na Rais Magufuli kimeshindikana, hata ahadi ya Prof. Ndalichako ya kuwalipa wanafunzi kabla ya 08 Agosti mwaka huu imeshindika lakini pia hata ahadi ya HESLB kuwalipa wanafunzi hao nusu ya fedha kabla ya kuanza kwa mafunzo hayo imeshindikana.
Wanafunzi wanasisitizwa kwenda katika vituo vyao vya mafunzo kwa vitendo huku wakiwa hawana fedha za kujikimu.
Nauli wanatoa wapi? Pengine wanatembea kwa miguu na kuomba lifti. Wanakula nini na kwa gharama za nani? Pengine wanashinda njaa na kuomba wenyeji wao katika vituo vyao wawape msaada au wanakula ‘nyasi’ kama ilivyopata kusemwa huko nyuma.

Comments

Popular posts from this blog

Kifafa cha Mimba (Preeclampsia, eclampsia)

MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes Kifafa cha mimba ni ugonjwa unaohusiana na msukumo mkubwa wa damu (high blood pressure) wakati wa ujauzito pamoja na kuharibika kwa viungo muhimu mwilini kama vile figo na ini. Kwa kawaida ugonjwa huu hutokea baada ya nusu ya kwanza ya ujauzito kuisha (kuanzia wiki ya 20 au miezi mitano ya ujauzito). Ugonjwa huu huweza kuwatokea hata wajawazito ambao hawakuwa na tatizo la msukumo mkubwa wa damu kabla ya ujauzito. Ugonjwa wa kifafa cha mimba unaweza kuleta madhara makubwa kwa mjamzito na mtoto aliye tumboni. Kuharibika kwa viungo muhimu kama figo na ini la mjamzito kunaweza kuwa kwa kiwango kikubwa kichoweza kusababisha mjamzito kupoteza maisha iwapo hatapata huduma ya afya mapema. Vilevile mtoto aliye tumboni anaweza kuathirika kwa kukosa damu ya kutosha toka kwa mama na kushindwa kukua vizuri na iwapo hali hiyo ikiendelea muda mrefu anaweza kufia tumboni. Kutokana na hatari kubwa ya ugonjwa huu kwa wajawazito na watoto walio tumboni, ina...

Medical gamble that saved a little boy’s life

  The 18-month old boy was rushed to Muhimbili National Hospital (MNH) in Dar es Salaam where he was admitted. But his condition soon deteriorated into acute kidney failure. A dark cloud hovered over the family. The country’s biggest referral hospital has for years been infamous for being too ill-equipped to save those dying from such conditions. To read the whole story click here

Haya ndiyo madhara ya Kutumia earphones

Imeelezwa kuwa watu wanaotumia redio za simu wako hatarini kupatwa na ugonjwa wa saratani ya sikio na kichwa kutokana na mionzi mikali itokanayo na viselula hivyo. Akizungumza na FICHUO TZ, Dk. Leopard Mwinuka alisema, watakaoathirika na tatizo hilo ni wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikioni ‘headphone’. “Nawaonea huruma wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikio, kwani madhara yake hawawezi kuyaona sasa bali siku zijazo watapata ugonjwa wa saratani,” alisema Dk. Mwinuka. Alimaliza kwa kusema kuwa, mbali na kupata ugonjwa huo, wahusika wanaweza kupata tatizo la kutosikia vizuri kwa sababu, mtu anapotumia spika za sikio huweka sauti kubwa ili apate mdundo mzuri baada ya muda ngoma ya sikio inaathiriwa na hali hiyo. Habari nyingine za kitabibu zilisema kwamba, kwa kuwa pande zote za spika zina sumaku, huweza kuvutana na kuvuruga mpangilio wa ubongo hasa kama spika hizo zitakaa maskioni kwa zaidi ya sa...