Skip to main content

Wauguzi 13 watumbuliwa Kalambo


MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes

HALMASHAURI ya Wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa, imewaondoa wauguzi 13 kwenye orodha ya malipo baada ya kubainika kuwa wana vyeti feki.

Aidha, Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo, limemfukuza kazi na kumtoa kwenye orodha ya malipo mhudumu wa zahanati iliyopo kijijini Mkombo, Winfrida Ngulo baada ya kukiri kuwa vyeti alivyokuwa navyo ni feki.

Pia madiwani wameagiza muuguzi Daraja la Pili aliyekuwa akifanya kazi kwenye zahanati hiyo ya Mkombo, Fatuma Efanga anayetuhumiwa kutoroka na zaidi ya Sh 700,000 zikiwa ni michango ya Mfuko wa Bima ya Afya ya Jamii (CHF) zilizochangwa na kaya maskini ili wahudumiwe kwenye zahanati hiyo.

Muuguzi huyo inadaiwa alikimbia na fedha hizo baada ya kubainika kuwa na vyeti feki.

Baraza hilo lililazimika kukaa kama kamati ili kumjadili na kumtolea maamuzi mhudumu huyo Ngulo ambaye inadaiwa alipofikishwa mbele ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) alikiri kuwa na vyeti feki .

Awali akichangia kwenye kikao cha baraza hilo, Diwani Mwachusa Sinjela alitahadharisha kuwa watumishi hewa na wenye vyeti feki wakipata taarifa kuwa wamebainika wamekuwa wakitoroka na kusababisha hasara.

“Mfano ninao kuna mtumishi wa afya (Fatuma) kwenye kata yangu nimepata taarifa kuwa ametoroka kituoni na fedha za michango ya CHF kiasi cha Sh 700,000 na hajulikani alikojificha,” alidai Sinjela.

Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, Dk Arcado Mwamba alisema orodha yote ya kaya maskini waliochanga fedha hizo CHF ipo na inafahamika. Kwa mujibu wa Dk Mwamba, zahanati hiyo ya Mkombo ilikuwa na watumishi wawili tu, Efanga na Ngulo ambao walikuwa wakitoa huduma.

“Kwa mantiki hiyo, zahanati hiyo kwa sasa haina mhudumu yeyote wa afya ila tuko mbioni kuwapeleka huko wahudumu wengine wa afya,” alieleza Dk Mwamba.

Akizungumza na gazeti hili nje ya baraza hilo, Ofisa Utumishi na Utawala wa halmashauri hiyo, John Maholani alisema wauguzi wa afya 13 wameondolewa kwenye orodha ya malipo baada ya kubainika kuwa wana vyeti feki.

Comments

Popular posts from this blog

Kifafa cha Mimba (Preeclampsia, eclampsia)

MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes Kifafa cha mimba ni ugonjwa unaohusiana na msukumo mkubwa wa damu (high blood pressure) wakati wa ujauzito pamoja na kuharibika kwa viungo muhimu mwilini kama vile figo na ini. Kwa kawaida ugonjwa huu hutokea baada ya nusu ya kwanza ya ujauzito kuisha (kuanzia wiki ya 20 au miezi mitano ya ujauzito). Ugonjwa huu huweza kuwatokea hata wajawazito ambao hawakuwa na tatizo la msukumo mkubwa wa damu kabla ya ujauzito. Ugonjwa wa kifafa cha mimba unaweza kuleta madhara makubwa kwa mjamzito na mtoto aliye tumboni. Kuharibika kwa viungo muhimu kama figo na ini la mjamzito kunaweza kuwa kwa kiwango kikubwa kichoweza kusababisha mjamzito kupoteza maisha iwapo hatapata huduma ya afya mapema. Vilevile mtoto aliye tumboni anaweza kuathirika kwa kukosa damu ya kutosha toka kwa mama na kushindwa kukua vizuri na iwapo hali hiyo ikiendelea muda mrefu anaweza kufia tumboni. Kutokana na hatari kubwa ya ugonjwa huu kwa wajawazito na watoto walio tumboni, ina...

Medical gamble that saved a little boy’s life

  The 18-month old boy was rushed to Muhimbili National Hospital (MNH) in Dar es Salaam where he was admitted. But his condition soon deteriorated into acute kidney failure. A dark cloud hovered over the family. The country’s biggest referral hospital has for years been infamous for being too ill-equipped to save those dying from such conditions. To read the whole story click here

Haya ndiyo madhara ya Kutumia earphones

Imeelezwa kuwa watu wanaotumia redio za simu wako hatarini kupatwa na ugonjwa wa saratani ya sikio na kichwa kutokana na mionzi mikali itokanayo na viselula hivyo. Akizungumza na FICHUO TZ, Dk. Leopard Mwinuka alisema, watakaoathirika na tatizo hilo ni wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikioni ‘headphone’. “Nawaonea huruma wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikio, kwani madhara yake hawawezi kuyaona sasa bali siku zijazo watapata ugonjwa wa saratani,” alisema Dk. Mwinuka. Alimaliza kwa kusema kuwa, mbali na kupata ugonjwa huo, wahusika wanaweza kupata tatizo la kutosikia vizuri kwa sababu, mtu anapotumia spika za sikio huweka sauti kubwa ili apate mdundo mzuri baada ya muda ngoma ya sikio inaathiriwa na hali hiyo. Habari nyingine za kitabibu zilisema kwamba, kwa kuwa pande zote za spika zina sumaku, huweza kuvutana na kuvuruga mpangilio wa ubongo hasa kama spika hizo zitakaa maskioni kwa zaidi ya sa...