Skip to main content

UFAULU KIDATO CHA SITA ULAYAS SECONDARY WILAYANI LUDEWA WASHUKA

UFAULU KIDATO CHA SITA ULAYAS SECONDARY WILAYANI LUDEWA WASHUKA
Muonekano wa Jengo la Utawala Ulayas Secondary
 


Mwl. Masoli Mkuu wa SHule Ulayas Sekondary Ludewa
                   Mwl. Timoth Haule Mwalimu mwandamizi Taaluma Ulayas Secondary Ludewa                       Mwl. Phoady Ngoloka mwalimu wa Nidhamu Ulayas Secondary Ludewa            Na Maiko Luoga Ludewa. Shule ya Sekodari Ulayasi Iliyopo katika kata ya Mlangali wilayani ludewa katika Mkoa Wa Njombe yenye Kidato cha kwanza hadi cha sita Imekuwa ikisifika kwa Umahiri wake Wa Kufaulisha zaidi wanafunzi na kupokea wanafunzi kutoka Maeneo Tofauti ya Nchi lakini Hivi karibuni Shule hiyo imeripotiwa kufanya vibaya Kwa upande Wa Taaluma sababu kubwa ikiwa ni Ubovu Wa nidhamu kwa wanafunzi Wa Shule hiyo. Siku chache baada ya Serikali Kutangaza Matokeo ya Kidato cha sita nchini Kwa mwaka huu 2016 Nimefika katika Shule ya Secondary Ulayasi Iliyopo Eneo la Mlangali ndani Wilayani Ludewa  Nakuzungumza na Baadhi ya walimu Akiwemo Mkuu Wa Shule hiyo Mwalimu Hashimu Masoli Ambaye ameyaweka Bayana matokeo ya Kidato cha Sita mwaka 2016 katika Shule yake ya Secondary Ulayasi ambapo yanaonesha kuwa Division One zipo 10, Division Two zipo 53, Division Three Zipo 72 Huku Division For zikiwa 11 na Division Zero ni 3. Hatahivyo Mwalimu huyo Ameongeza kuwa Shule yake imeshika nafasi ya pili Kiwilaya Kati Ya shule mbili za A -Level zilizopo wilayani Ludewa Huku ikishika Nafasi ya 11 Kimkoa kati ya shule 11 za mkoa Wa Njombe na Kitaifa Shule hiyo ni ya 312 kati Ya Shule 423 Hivyo matokeo hayo yameifanya shule ya Secondary Ulayasi Kushuka Kitaaluma kwa Mwaka huu Ukilinganisha na Mwaka 2015 Ambapo Mwalimu Masoli amesema Hiyo imesababishwa na Tabia mbaya waliyokuwa nayo Baadhi ya wanafunzi ya Kufanya vurugu Mwaka 2015 Wakati Shule hiyo ikisimamiwa na Mwalimu Mkuu mwingine tofauti na yeye. Mwalimu Phoady Ngoloka Ni Mwalimu Wa Nidhamu Katika Shule ya Ulayasi Secondary Amesema kuwa Hapo mwanzo Wanafunzi Wa shule hiyo walikuwa hawana nidhamu Bora  Hali iliyosababisha Shule hiyo kufanya Vibaya katika Matokeo ya Kidato cha Sita Mwaka huu 2016 Hivyo mara baada ya Kulibaini tatizo hilo wao Kama Bodi ya Shule wamepanga Kuimarisha Nidhamu kwa wanafunzi ili kuweza kutoa matokeo Mazuri ya Kidato cha sita ifikapo mwaka 2017 na Kurudisha Hadhi ya Ulayas Secondary iliyotawala Miaka Mingi iliyopita. Naye mwalimu Mwandamizi Wa Taaluma katika Shule hiyo aliyejitambulisha kwa jina la Thimoth HauleAmekiri kufanya Vibaya Katika Matokeo hayo ya kidato Cha Sita na kwamba Hayairidhishi jamii ya Watanzania Hivyo Wao wameliona Tatizo hilo na kuamua kujipanga katika kufundisha kwa bidii Na kumubana kila mwalimu Kuhakikisha anafundisha Vipindi vyake Kwa ufasaha ikiwa ni pamoja na Kuongeza walimu wakujitolea ili waweze Kuziba Pengo la Walimu katika shule yao. Kwaupande wake Diwani Wa Kata Ya Mlangali ilipo Shule hiyo Mh. Khamis Kayombo amesema kuwa amefanya kikao na Mkuu Wa Shule hiyo na kumuagiza Kuanza kubadilika Maramoja katika utendaji kazi wao Huku akiwaaminisha wananchi Wa Tanzania kuwa Sasa Mkakati maalumu Umewekwa Hivyo waamini Shule 

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

Kifafa cha Mimba (Preeclampsia, eclampsia)

MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes Kifafa cha mimba ni ugonjwa unaohusiana na msukumo mkubwa wa damu (high blood pressure) wakati wa ujauzito pamoja na kuharibika kwa viungo muhimu mwilini kama vile figo na ini. Kwa kawaida ugonjwa huu hutokea baada ya nusu ya kwanza ya ujauzito kuisha (kuanzia wiki ya 20 au miezi mitano ya ujauzito). Ugonjwa huu huweza kuwatokea hata wajawazito ambao hawakuwa na tatizo la msukumo mkubwa wa damu kabla ya ujauzito. Ugonjwa wa kifafa cha mimba unaweza kuleta madhara makubwa kwa mjamzito na mtoto aliye tumboni. Kuharibika kwa viungo muhimu kama figo na ini la mjamzito kunaweza kuwa kwa kiwango kikubwa kichoweza kusababisha mjamzito kupoteza maisha iwapo hatapata huduma ya afya mapema. Vilevile mtoto aliye tumboni anaweza kuathirika kwa kukosa damu ya kutosha toka kwa mama na kushindwa kukua vizuri na iwapo hali hiyo ikiendelea muda mrefu anaweza kufia tumboni. Kutokana na hatari kubwa ya ugonjwa huu kwa wajawazito na watoto walio tumboni, ina...

Medical gamble that saved a little boy’s life

  The 18-month old boy was rushed to Muhimbili National Hospital (MNH) in Dar es Salaam where he was admitted. But his condition soon deteriorated into acute kidney failure. A dark cloud hovered over the family. The country’s biggest referral hospital has for years been infamous for being too ill-equipped to save those dying from such conditions. To read the whole story click here

Haya ndiyo madhara ya Kutumia earphones

Imeelezwa kuwa watu wanaotumia redio za simu wako hatarini kupatwa na ugonjwa wa saratani ya sikio na kichwa kutokana na mionzi mikali itokanayo na viselula hivyo. Akizungumza na FICHUO TZ, Dk. Leopard Mwinuka alisema, watakaoathirika na tatizo hilo ni wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikioni ‘headphone’. “Nawaonea huruma wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikio, kwani madhara yake hawawezi kuyaona sasa bali siku zijazo watapata ugonjwa wa saratani,” alisema Dk. Mwinuka. Alimaliza kwa kusema kuwa, mbali na kupata ugonjwa huo, wahusika wanaweza kupata tatizo la kutosikia vizuri kwa sababu, mtu anapotumia spika za sikio huweka sauti kubwa ili apate mdundo mzuri baada ya muda ngoma ya sikio inaathiriwa na hali hiyo. Habari nyingine za kitabibu zilisema kwamba, kwa kuwa pande zote za spika zina sumaku, huweza kuvutana na kuvuruga mpangilio wa ubongo hasa kama spika hizo zitakaa maskioni kwa zaidi ya sa...