Skip to main content

MADHARA YA KUNYWA POMBE KIPINDI CHA UJAUZITO

 
Kipindi cha ujauzito kwa mama ni kipindi muhimu sana ambacho kwa wakati huu mama hatakiwi atumie kitu chochote cha kujitibu bila ushauri wa daktari kwani kinaweza kudhuru mtoto lakini pia kipindi cha ujauzito ni kipindi ambacho mama hatakiwi kunywa kileo chochote kile unachokifahamu.

Sio bia, sio spirit, wala mvinyo au wine. wanawake wengi wa siku hizi hubeba mimba bila kufahamu kwamba wana mimba na huja kugundua baada ya mwezi mmoja au miwili baada ya kumshindilia mtoto pombe za kutosha.tabia hii ina madhara makubwa sana kwa mama na mtoto kama ifuatavyo...

1. Mtoto kua na umbo la ajabu; mtoto huweza kuzaliwa na kichwa kidogo, uso kama bapa na macho madogo sana. dalili hizi huweza kuanza kuonekana katika umri wa miaka 2 na mara nyingi mtoto hua tofauti na wenzake.


2. Kuchelewa kukua; pombe huingilia mfumo wa ukuaji na kumchelewesha mtoto kufanya baadhi ya mambo kama kutambaa, kutembea, kuongea na kadhalika. ukimuangalia mtoto mwenye umri kama huo huo ataonekana mkubwa kuliko huyu anayetumia pombe.

3. Kushindwa kujifunza; mara nyingi watoto hawa hua wabovu sana darasani na kushindwa kuelewa vitu kama watoto wengine..mata nyingi mzazi huishia kulalamika na kumshangaa mtoto na kumuona mzembe bila kujua chanzo ni yeye...

4. Kuchelewa kula kwa mtoto; kawaida mtoto anatakiwa anywe maziwa tu kwa muda wa miezi sita, tena maziwa ya mama baada ya hapo aanze kula chakula. mtoto aliyepata madhara ya pombe hushindwa kunyonya na kuchukua muda mrefu sana kuanza kula.

5. Matatizo ya viungo; siku hizi kuna picha zinatumwa sana mitandaoni zikionyesha mtoto kazaliwa bila mikono, miguu au kaunganikana kichwa na pacha mwenzake. hizo sio bahati mbaya kama watu wanavyodhani ila hayo ni madhara ya vitu ikiwemo pombe.

6. Kuharibika kwa ujauzito; pombe inaweza kuingilia mfumo wa homoni za mwanamke au kufungua mlango wa uzazi na kusababisha kuharibika kwa mimba, mimba huweza kuharibika ghafla au taratibu kulingana na aina ya pombe.

7. Kuzaa kabla ya muda; kwenye mimba kubwa pombe inaweza kusababisha kuanza kwa uchungu kabla ya muda na kumzaa mtoto ambaye hajakomaa maarufu kama kabichi.

Mwisho; hakuna kipindi ambacho ni salama kunywa pombe kipindi cha ujauzito, kama hauhitaji mtoto kwa sasa tumia vizuizi vya mimba lakini kama unakunywa pombe na kufanya ngono bila kinga utajikuta una mimba ambayo imeshaathirika na pombe tayari na ukipata mimba acha pombe kabisa.

Comments

Popular posts from this blog

Kifafa cha Mimba (Preeclampsia, eclampsia)

MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes Kifafa cha mimba ni ugonjwa unaohusiana na msukumo mkubwa wa damu (high blood pressure) wakati wa ujauzito pamoja na kuharibika kwa viungo muhimu mwilini kama vile figo na ini. Kwa kawaida ugonjwa huu hutokea baada ya nusu ya kwanza ya ujauzito kuisha (kuanzia wiki ya 20 au miezi mitano ya ujauzito). Ugonjwa huu huweza kuwatokea hata wajawazito ambao hawakuwa na tatizo la msukumo mkubwa wa damu kabla ya ujauzito. Ugonjwa wa kifafa cha mimba unaweza kuleta madhara makubwa kwa mjamzito na mtoto aliye tumboni. Kuharibika kwa viungo muhimu kama figo na ini la mjamzito kunaweza kuwa kwa kiwango kikubwa kichoweza kusababisha mjamzito kupoteza maisha iwapo hatapata huduma ya afya mapema. Vilevile mtoto aliye tumboni anaweza kuathirika kwa kukosa damu ya kutosha toka kwa mama na kushindwa kukua vizuri na iwapo hali hiyo ikiendelea muda mrefu anaweza kufia tumboni. Kutokana na hatari kubwa ya ugonjwa huu kwa wajawazito na watoto walio tumboni, ina...

Medical gamble that saved a little boy’s life

  The 18-month old boy was rushed to Muhimbili National Hospital (MNH) in Dar es Salaam where he was admitted. But his condition soon deteriorated into acute kidney failure. A dark cloud hovered over the family. The country’s biggest referral hospital has for years been infamous for being too ill-equipped to save those dying from such conditions. To read the whole story click here

Haya ndiyo madhara ya Kutumia earphones

Imeelezwa kuwa watu wanaotumia redio za simu wako hatarini kupatwa na ugonjwa wa saratani ya sikio na kichwa kutokana na mionzi mikali itokanayo na viselula hivyo. Akizungumza na FICHUO TZ, Dk. Leopard Mwinuka alisema, watakaoathirika na tatizo hilo ni wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikioni ‘headphone’. “Nawaonea huruma wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikio, kwani madhara yake hawawezi kuyaona sasa bali siku zijazo watapata ugonjwa wa saratani,” alisema Dk. Mwinuka. Alimaliza kwa kusema kuwa, mbali na kupata ugonjwa huo, wahusika wanaweza kupata tatizo la kutosikia vizuri kwa sababu, mtu anapotumia spika za sikio huweka sauti kubwa ili apate mdundo mzuri baada ya muda ngoma ya sikio inaathiriwa na hali hiyo. Habari nyingine za kitabibu zilisema kwamba, kwa kuwa pande zote za spika zina sumaku, huweza kuvutana na kuvuruga mpangilio wa ubongo hasa kama spika hizo zitakaa maskioni kwa zaidi ya sa...