Skip to main content

Muhimbili kutumia mitandao ya simu kulipia huduma


MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) inatarajia kuanza kutumia mitandao ya simu, kadi maalimu na kadi za benki kwa ajili ya kulipia huduma za matibabu ili kudhibiti changamoto za upotevu wa fedha na wizi katika ukusanyaji wa mapato ya hospitali hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma na Huduma kwa Wateja, Bw Aminiel Eligaesha, hospitali hiyo imelenga pia kuimarisha njia za ukusanyaji mapato ili kuboresha huduma za matibabu na kuboresha maslahi kwa wafanyakazi.
Amesema mpango wa kutumia njia za kieletroniki umelenga kukusanya mapato zaidi ili kuiwezesha hospitali hiyo kukabiliana na changamoto mbalimbali za uendeshaji na kutoa huduma bora kwa wagonjwa.
Lengo la hospitali hiyo ni kuongeza mapato na kupunguza matumizi na kutengeneza mazingira ya kujiendesha na kutoa huduma bora kwa wagonjwa mbalimbali nchini.
“Hospitali imelenga kuboresha wadi za kulaza wagonjwa wanaohitaji huduma na malazi binafsi, kuhakikisha wagonjwa wanachangia huduma za matibabu na kuboresha mfumo wa kuandaa hati za madai kwa kampuni na mifuko ya Taifa ya bima ya afya.
Taarifa hiyo imeeleza kwamba hospitali hiyo imedhamiria pia kutoa motisha kwa wafanyakazi wengine ili kuongeza ufanisi katika maeneo yao ya kazi.
Katika hatua nyingine, hospitali hiyo imeweka mikakati ya kupunguza gharama za kununua dawa na vifaa tiba kutoka viwandani (Manufacturers) moja kwa moja.
“Kwa mfano, baada ya kupata kibali kutoka TFDA, Hospitali imenunua dawa za figo (immunosuppressant) kutoka India kwa Sh 226 milioni wakati hapa nchini zingegharimu Sh 500 milioni,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Pia, hospitali hiyo imeagiza nyuzi za kushonea wagonjwa (sutures) kutoka kiwandani (Ethicon) kwa gharama ya Sh 321 milioni wakati zingegharimu Sh 668 milioni endapo zingenunuliwa nchini.
Katika taarifa hiyo imebainisha kuwa hospitali hiyo imeweza kupunguza gharama za uchujaji wa damu (dialysis) kutoka wastani wa Sh 250,000 kwa kila zamu (session) hadi kufikia Sh171,000.

Comments

Popular posts from this blog

Kifafa cha Mimba (Preeclampsia, eclampsia)

MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes Kifafa cha mimba ni ugonjwa unaohusiana na msukumo mkubwa wa damu (high blood pressure) wakati wa ujauzito pamoja na kuharibika kwa viungo muhimu mwilini kama vile figo na ini. Kwa kawaida ugonjwa huu hutokea baada ya nusu ya kwanza ya ujauzito kuisha (kuanzia wiki ya 20 au miezi mitano ya ujauzito). Ugonjwa huu huweza kuwatokea hata wajawazito ambao hawakuwa na tatizo la msukumo mkubwa wa damu kabla ya ujauzito. Ugonjwa wa kifafa cha mimba unaweza kuleta madhara makubwa kwa mjamzito na mtoto aliye tumboni. Kuharibika kwa viungo muhimu kama figo na ini la mjamzito kunaweza kuwa kwa kiwango kikubwa kichoweza kusababisha mjamzito kupoteza maisha iwapo hatapata huduma ya afya mapema. Vilevile mtoto aliye tumboni anaweza kuathirika kwa kukosa damu ya kutosha toka kwa mama na kushindwa kukua vizuri na iwapo hali hiyo ikiendelea muda mrefu anaweza kufia tumboni. Kutokana na hatari kubwa ya ugonjwa huu kwa wajawazito na watoto walio tumboni, ina...

Medical gamble that saved a little boy’s life

  The 18-month old boy was rushed to Muhimbili National Hospital (MNH) in Dar es Salaam where he was admitted. But his condition soon deteriorated into acute kidney failure. A dark cloud hovered over the family. The country’s biggest referral hospital has for years been infamous for being too ill-equipped to save those dying from such conditions. To read the whole story click here

Haya ndiyo madhara ya Kutumia earphones

Imeelezwa kuwa watu wanaotumia redio za simu wako hatarini kupatwa na ugonjwa wa saratani ya sikio na kichwa kutokana na mionzi mikali itokanayo na viselula hivyo. Akizungumza na FICHUO TZ, Dk. Leopard Mwinuka alisema, watakaoathirika na tatizo hilo ni wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikioni ‘headphone’. “Nawaonea huruma wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikio, kwani madhara yake hawawezi kuyaona sasa bali siku zijazo watapata ugonjwa wa saratani,” alisema Dk. Mwinuka. Alimaliza kwa kusema kuwa, mbali na kupata ugonjwa huo, wahusika wanaweza kupata tatizo la kutosikia vizuri kwa sababu, mtu anapotumia spika za sikio huweka sauti kubwa ili apate mdundo mzuri baada ya muda ngoma ya sikio inaathiriwa na hali hiyo. Habari nyingine za kitabibu zilisema kwamba, kwa kuwa pande zote za spika zina sumaku, huweza kuvutana na kuvuruga mpangilio wa ubongo hasa kama spika hizo zitakaa maskioni kwa zaidi ya sa...