Skip to main content

Mikojo ya walevi kutumika kutengenezea bia


MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes

GHENT, Ubeligiji
WATUMIAJI wa pombe sasa wataweza kupata auheni ya bei ya vinywaji hivyo, baada ya wanasayansi kugundua kifaa maalumu kitakachotumika kubadilisha mikojo ya walevi kutumika kutengenezea bia.

Kugunduliwa kwa kifaa hicho ni mkombozi kwa wamiliki wa viwanda vya pombe ambapo wataweza kupata malighafi ya kutengenezea bia kwa urais.

Kinatarajiwa kufungwa kwenye vyoo vya baa mbalimbali ili kurahisisha upatikanaji wa mikojo hiyo ya walevi.

Kifaa hicho ambacho kitakuwa kikitumia umeme wa jua pia kitakuwa na uwezo wa kubadili mikojo hiyo kutumika kama maji ya kunywa.

Timu ya watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Ghent nchini Ubeligiji, walisema kifaa hicho kitaanza kutumika hususan maeneo ya mijini kwenye nchi zinazoendelea.

Licha ya kuwepo kwa mashine maalum yenye uwezo wa kutibu maji machafu ikiwemo mkojo kisha kutumika kwa matumizi mengine muhimu ya binaadamu, wataalamu hao wamesema kifaa hicho walichokigundua kinauwezo zaidi wa kuyatibu maji hayo bila kutumia nguvu ya umeme.

Dk. Sebastiaan Derese, alisema kifaa hicho kitakuwa kikitunza mikojo kwenye tangi maalum ambalo litatumika kutibu kisha kutumika kama malighafi ya kutengenezea bia.

Kwa mara ya kwanza kifaa hicho kilianza kutumika kwenye tamasha la muziki ililofanyika mjini humo ambapo jumla ya lita 1000 za mikojo, zilikusanywa kisha kutengenezewa bia.

Alibainisha kuwa, bia zilizotengenezwa kupitia mikojo hiyo imewavutia wanywaji wengi hususan kwenye matamasha mbalimbali.

Comments

Popular posts from this blog

Kifafa cha Mimba (Preeclampsia, eclampsia)

MTU KWAO BLOG / Eagle Eyes Kifafa cha mimba ni ugonjwa unaohusiana na msukumo mkubwa wa damu (high blood pressure) wakati wa ujauzito pamoja na kuharibika kwa viungo muhimu mwilini kama vile figo na ini. Kwa kawaida ugonjwa huu hutokea baada ya nusu ya kwanza ya ujauzito kuisha (kuanzia wiki ya 20 au miezi mitano ya ujauzito). Ugonjwa huu huweza kuwatokea hata wajawazito ambao hawakuwa na tatizo la msukumo mkubwa wa damu kabla ya ujauzito. Ugonjwa wa kifafa cha mimba unaweza kuleta madhara makubwa kwa mjamzito na mtoto aliye tumboni. Kuharibika kwa viungo muhimu kama figo na ini la mjamzito kunaweza kuwa kwa kiwango kikubwa kichoweza kusababisha mjamzito kupoteza maisha iwapo hatapata huduma ya afya mapema. Vilevile mtoto aliye tumboni anaweza kuathirika kwa kukosa damu ya kutosha toka kwa mama na kushindwa kukua vizuri na iwapo hali hiyo ikiendelea muda mrefu anaweza kufia tumboni. Kutokana na hatari kubwa ya ugonjwa huu kwa wajawazito na watoto walio tumboni, ina...

Medical gamble that saved a little boy’s life

  The 18-month old boy was rushed to Muhimbili National Hospital (MNH) in Dar es Salaam where he was admitted. But his condition soon deteriorated into acute kidney failure. A dark cloud hovered over the family. The country’s biggest referral hospital has for years been infamous for being too ill-equipped to save those dying from such conditions. To read the whole story click here

Haya ndiyo madhara ya Kutumia earphones

Imeelezwa kuwa watu wanaotumia redio za simu wako hatarini kupatwa na ugonjwa wa saratani ya sikio na kichwa kutokana na mionzi mikali itokanayo na viselula hivyo. Akizungumza na FICHUO TZ, Dk. Leopard Mwinuka alisema, watakaoathirika na tatizo hilo ni wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikioni ‘headphone’. “Nawaonea huruma wanaotumia muda mwingi kusikiliza redio ama muziki kwa kutumia spika za masikio, kwani madhara yake hawawezi kuyaona sasa bali siku zijazo watapata ugonjwa wa saratani,” alisema Dk. Mwinuka. Alimaliza kwa kusema kuwa, mbali na kupata ugonjwa huo, wahusika wanaweza kupata tatizo la kutosikia vizuri kwa sababu, mtu anapotumia spika za sikio huweka sauti kubwa ili apate mdundo mzuri baada ya muda ngoma ya sikio inaathiriwa na hali hiyo. Habari nyingine za kitabibu zilisema kwamba, kwa kuwa pande zote za spika zina sumaku, huweza kuvutana na kuvuruga mpangilio wa ubongo hasa kama spika hizo zitakaa maskioni kwa zaidi ya sa...